Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Daraja Kata ya Arusha chini litakalounganisha Vijiji vya Muungano, Mikocheni na Chemchem?

Supplementary Question 1

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Nina maswali mawili ya nyongeza. Barabara ya Getifonga - Mabogini hadi Kahe, iko kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi kujengwa kwa kiwango cha lami na huko ndiko ilikojengwa hospitali ya wilaya: Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara hii?

Mheshimiwa Spika, barabara ya International School - Kibosho KCU hadi kwa Raphael imebakiza kilomita nane kukamilika kwa kiwango cha lami: Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara hii?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Profesa Patrick Alois Ndakidemi, Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba barabara aliyoitaja mwanzo ya kutoka Getifonga – Mabogini Kahe, ipo katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge barabara hii kwa sasa iko katika usanifu kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa kiwango cha lami. Usanifu unaofanyika ni wa kilomita 31.25, kwa hiyo, tupo katika hatua nzuri kwenye hiyo.

Mheshimiwa Spika, barabara ya kutoka International School – Kibosho - KNCU mpaka kwa Raphael na yenyewe kilomita 8.42 tayari imeshajengwa kwa kiwango cha lami. Kiwango ambacho kimebakia ni kilomita 5.49, kwa hiyo na yenyewe tunatafuta fedha ili tuanze ujenzi kwa kiwango hicho.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Daraja Kata ya Arusha chini litakalounganisha Vijiji vya Muungano, Mikocheni na Chemchem?

Supplementary Question 2

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nataka kuuliza ni lini sasa Serikali itajenga daraja linalounganisha Halmashauri ya Msalala, Kijiji cha Namba Tisa na Halmashauri ya Nyang’hwale? Ahsante sana.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, Mbunge wa Jimbo la Msalala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja ya kazi kubwa ambayo sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI tumekubaliana kuifanya sasa ni pamoja na kutambua madaraja korofi yote ambayo tunahitaji kuyahudumia sasa ili tuunganishe moja na eneo lingine. Kwa hiyo, hata hili daraja alilotaja Mheshimiwa Mbunge la kuunganisha Halmashauri ya Msalala na Halmashauri ya Nyang’hwale liko katika mpango wetu, hivyo, nimuondoe hofu katika hilo.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Daraja Kata ya Arusha chini litakalounganisha Vijiji vya Muungano, Mikocheni na Chemchem?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza niipongeze Wizara kupitia TAMISEMI, kupeleka fedha nyingi katika Kata ya Swaya. Naomba kujua kama ni lini watawaongezea ili waweze kujenga daraja linalounganisha wananchi na hasa wanafunzi kuelekea kwenye Shule ya Sekondari ya Swaya?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumekuwa tukipeleka fedha mara kwa mara, uzuri yeye mwenyewe amekuwa ni shuhuda na nimhakikishie tu kwamba sisi tunazingatia maoni ya wananchi na jambo lake tumelipokea. Ahsante sana.