Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 41 2022-11-03

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kujenga Daraja Kata ya Arusha chini litakalounganisha Vijiji vya Muungano, Mikocheni na Chemchem?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Prof. Patrick Alois Ndakidemi, Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 barabara hii imetengewa fedha kiasi cha Shilingi milioni 475.00 kwa ajili ya kuanza kujenga daraja katika Mto Ronga ili kuweza kuunganisha Vijiji vya Muungano, Mikocheni na Chemchem. Mradi huu upo katika hatua za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TARURA itaendelea kuweka katika vipaumbele vyake ujenzi wa barabara hii kulingana na upatikanaji wa fedha ili kuhakikisha inaweza kupitika katika kipindi chote cha mwaka.