Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA K.n.y. MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Mkalama?

Supplementary Question 1

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kuweza kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Wilaya ya Mkalama ina gari mmoja ambalo pia ni bovu.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba, wanapomaliza ujenzi wa kituo hicho wanawapa na nyenzo kama magari na pikipiki maalum?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, katika Jimbo la Kalenga pia kuna kituo cha Polisi cha Kata ya Ifunda lakini hawana nyumba Askari hao na pia hawana magari, je, ni mkakati gani wa Serikali unao ili kuhakikisha kwamba kituo hiko kinapata nyumba za watumishi pamoja na magari? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Tendega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja, kuhusu Kituo cha Mkalama baada ya kukamilika kupewa nyenzo za kutendea kazi ikiwemo magari, hilo ni wazi, gari lililopo kama ni bovu, kituo kitakapokamilika tutawapa gari ili waweze kutimiza majukumu yao vizuri. Kwa bahati nzuri tumeanza kupokea magari hayo na yameanza kugawiwa kule ambako kuna mahitaji makubwa sana.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Kalenga, hii Kata ya Ifunda, kuwa na kituo ambacho hakina nyumba wala magari; tutawasiliana na uongozi wa Polisi wa Mkoa, nadhani ni Iringa hii, ili kuona kama wanalo eneo la kutosha basi waingize kwenye mpango wa ujenzi waweze kufikiriwa kujengewa. Nashukuru. (Makofi)

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA K.n.y. MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Mkalama?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Wilaya ya Mkalama pamoja na kuwa Kituo hicho kimekuwa gofu muda mrefu lakini pia Askari ni wachache sana, katika Kata zote 17 ambazo zinamtawanyiko mkubwa, sehemu kubwa tunatumia mgambo. Serikali inatuambia nini kuhusu kutupatia Askari wapya katika mgao unaokuja. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Francis Mtinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Wilaya nyingi hasa ambazo hazikuwa na Vituo vya Polisi, wamekuwa na Askari kulingana na uwezo wa vituo vilivyopo kuwabeba. Tunashukuru baada ya kupata ajira ya zaidi ya Askari 4,200 waliotoka kwenye mafunzo mwanzoni mwa mwaka huu, wameweza kugawiwa kwenye vituo hivi, vikiwemo mpaka ngazi za Kata. Naamini Mheshimiwa Francis anafahamu kwamba sasa hivi tunao Askari Kata ngazi ya Cheo cha Mkaguzi Msaidizi wa Polisi kwa ajili ya kusimamia usalama katika ngazi hizo. Kwa hiyo, naamini atakuwa amepata Askari hao kwenye Jimbo lake la Mkalama. Nashukuru.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA K.n.y. MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Mkalama?

Supplementary Question 3

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itamalizia Kituo cha Polisi cha Galapo ambacho iliahidi kwamba itatekeleza katika mwaka huu wa fedha 2022/2023?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daniel Sillo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kweli tumeshazungumza juu ya jambo hili na Mheshimiwa Sillo, nimeahidi baada ya Bunge hili kutembelea eneo lile la Galapo kwa sababu ni eneo ambalo ni kubwa sana kibiashara linahitaji Kituo cha Polisi. Tumeingiza kwenye mpango wa kukamilisha ujenzi wa kituo hicho ili wananchi wa eneo hilo waweze kupata huduma za usalama wa raia na mali zao.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA K.n.y. MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Mkalama?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wananchi wa Kata ya Nanjilinji katika Jimbo la Kilwa Kusini, wamekamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi wakishirikiana nami Mbunge wao. Je, Serikali iko tayari kutoa maelekezo kupitia Bunge hili kwa Uongozi wa Polisi Mkoa wa Lindi ili wakakague kituo hicho na hatimae kupeleka Askari Polisi pale Nanjilinji?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kassinge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza niwapongeze kwa kukamilisha ujenzi wa kituo hicho, hivyo ni wajibu wetu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi hususan Jeshi la Polisi, kupeleka Askari. Kupitia Bunge lako naomba kuelekeza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Lindi wafanye ukaguzi kama kinakidhi wa wapangie Askari ili waweze kutoa huduma za usalama wa raia kwenye eneo hili la Nanjilinji. Nashukuru sana.