Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 31 2022-11-02

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA K.n.y. MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Mkalama?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jesca David Kishoa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkalama ni Kituo cha Daraja A. Ujenzi wake ulianza mwezi Juni, 2015 na ulisimama kutokana na kukosekana kwa fedha. Katika Bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga kiasi cha Shilingi 467,148,000 ili kukamilisha ujenzi wa kituo hiko. Nashukuru.