Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kutoa kipaumbele cha ajira kwa Majeshi yote nchini kwa Vijana waliohitimu JKT?

Supplementary Question 1

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini na maswali mawili la nyongeza.

Swali la kwanza; agizo la Serikali kwa Wizara nyingine kutoa kipaumbele cha ajira kwa Vijana wa JKT limetekelezeka kwa kiwango gani tangu 2013?

Swali la pili; inafahamika kuwa malengo ya mafunzo ya JKT siyo ajira, bali ni kufundisha ujasiriamali na uzalendo. Je, Serikali haioni haja sasa kuaajiri kutoka JKT kwa kufuata mtiririko ule wa first in first out? Kwa maana operesheni ya mwanzo wawahi kuajiriwa kuliko wale wanaofuata ili kutovunja moyo vijana wetu wazalendo. (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Antipas Mgungusi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nianze na suala la first in first out, huu ndiyo utaratibu ambao unatumika, lakini wakati mwingine kunakuwa kuna uhitaji wa utaalam maalum au sifa maalum, kwa hiyo pamoja na kwamba mfumo wa first in first out unatumika, unaweza ukatumia mfumo huu lakini kundi la kwanza usipate watu wenye zile sifa maalum ambavyo Vyombo Vyetu vya Ulinzi na Usalama wanatafuta, kwa hiyo unalazimika kwenda kwenye kundi la pili.

Mheshimiwa Spika, hoja ya Mheshimiwa Mbunge nimeielewa na ndiyo maana hata Waheshimiwa Wabunge wengine wamepiga makofi wakiashiria kwamba ni swali la msingi. Kwa hiyo, tunachokifanya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, sasa hivi nimeunda Kamati ambayo tunashirikisha Wizara mbalimbali hasa Wizara ambazo ni productive sectors. Wizara ya Kilimo, tayari tunashirikiana nao ninamshukuru Mheshimiwa Bashe, upande wa Kilimo cha kimkakati, tunashirikiana na Jeshi la Kujenga Taifa.

Mheshimiwa Spika, tunataka tupanue mawanda au scope ya JKT kwa kushirikisha sekta nyingine. Kwa mfano, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo, Wizara ya Viwanda na Biashara na taasisi ambazo zipo chini ya Wizara hizi. Kwa mfano, SIDO, VETA, TIRDO, TEMDO lakini benki yetu ya TADB. Asilimia 10 za vikundi kwenye Halmashauri tukae pamoja kama Serikali tuwe na mkakati wa pamoja ambao utashirikisha Jeshi la Kujenga Taifa na Wizara hizi na Taasisi hizi ili kusaidia kutengeneza commitement ya ajira Milioni Nane ambazo tumeahidi kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi na kupitia Jeshi la Kujenga Taifa kwa sababu tunaandaa vijana kwenye kujifunza stadi za kazi, basi kwa mawanda hayo tunaweza tuka-absorb vijana wengi zaidi ambao wanamaliza mafunzo ya kujitolea wanarudi nyumbani. (Makofi)