Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 30 2022-11-02

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kutoa kipaumbele cha ajira kwa Majeshi yote nchini kwa Vijana waliohitimu JKT?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Antipas Zeno Mgungusi, Mbunge wa Malinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mnamo mwaka 2013 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilitoa maelekezo kwa Wizara zote pamoja na Vyombo vyote vya Ulinzi na Usalama kutoa kipaumbele cha ajira kwa vijana waliohitimu mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa. Utaratibu huo umekuwa ukitekelezwa na Vyombo vyote vya Ulinzi na Usalama kuanzia mwaka 2013 yalipotolewa maelekezo hayo. Aidha, inakumbushwa kuwa lengo la mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa ni kuwapatia vijana wa Tanzania elimu ya uzalendo, ujasiriamali na kujifunza stadi za kazi ili waweze kujiajiri mara wamalizapo mkataba. Ahsante sana.