Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JUSTINE L. NYAMOGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga bwawa la maji katika Kata ya Nyanzwa kwa ajili ya skimu ya umwagiliaji?

Supplementary Question 1

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Swali la kwanza; katika Kijiji cha Mgowelo ambacho kiko katika Kata hiyo hiyo ya Nyanzwa, kumetengwa zaidi ya hekta 3000 kwa ajili ya block farming. Je, Serikali iko tayari kufanya utafiti kwenye eneo hilo na kuona umuhimu wa kuweka skimu pia kwenye hilo eneo kwa sababu ni hekta nyingi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwenye Bunge lililopita, niliomba Naibu Waziri au Waziri kutembelea eneo hili na kuangalia changamoto tunazopata za skimu mbalimbali, lakini mpaka sasa ziara hiyo haijafanyika. Je, Waziri ananiahidi lini atafika Jimboni Kilolo kwa ajili ya kutembelea na kuona tunaweza tukashauriana vipi? Ahsante.

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, maswali yake mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kufika jimboni kwake naomba nimuahidi yeye na wananchi, nitakwenda mwenyewe baada ya Bunge hili kwa ajili ya kwenda kufanya kazi hiyo pamoja na kuangalia mwendelezo wa mradi wetu wa pamoja wa chai ambao yeye mwenyewe alikuwa muasisi wa kuanzisha huo mradi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu hii block farm, naomba nimwombe baada ya kikao cha Bunge tukutane ofisini ili nimkabidhi timu ya watu ambao wataenda kufanya soil analysis na kuchukua mipaka ili tuiweke kwenye mipango ya Wizara.

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. JUSTINE L. NYAMOGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga bwawa la maji katika Kata ya Nyanzwa kwa ajili ya skimu ya umwagiliaji?

Supplementary Question 2

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Serikali ilituahidi kwamba mwezi wa Saba tungepata consultant kwa ajili ya Bwawa kubwa la Mkomazi, lakini mpaka leo kuna ukimya. Je, ni lini ahadi hii itatekelezwa?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Mnzava, kuhusu Bwawa la Mkomazi yeye mwenyewe anafahamu hivi karibuni timu ya Wizara ya Kilimo ilikuwepo kule na tatizo lililokuwepo katika suala la Mkomazi, design iliyokuwa imefanyika toka awali na zile skimu zilizoko maeneo yale ilikuwa ina makosa. Kwa hiyo, wataalam wa Wizara wamefanya kazi ya kwanza kwa ajili ya kwenda kutembelea na kuangalia na nimuahidi tu yeye na wananchi wa jimbo lake, kwamba next financial year ya 2023, Bwawa la Mkomazi litakuwa kwenye miradi itakayojengwa na Wizara ya Kilimo kwa ajili ya eneo hilo na skimu zote zilizoko katika ukanda ule ambazo ziko saba.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUSTINE L. NYAMOGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga bwawa la maji katika Kata ya Nyanzwa kwa ajili ya skimu ya umwagiliaji?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itakarabati Bwawa la Nyangokorwa lililoko Wilaya ya Bariadi ili liweze kutumika katika kilimo cha umwagiliaji?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Midimu na Wabunge wote wa Mkoa wa Simiyu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara sasa hivi inachokifanya ni kuangalia namna gani tunaweza kutumia resource ya maji inayotoka katika Ziwa Victoria na kwa kuwa kuna Mradi wa Maji wa Ziwa Victoria, unayoyatoa maji Ziwa Victoria kuyaleta Mkoa wa Simiyu, sasa hivi tutashirikiana na wenzetu wa Wizara ya Maji, ili tuweze ku-tap yale maji yanayotoka Ziwa Victoria ili kuweza ku-develop skimu katika Mkoa wa Simiyu.

Mheshimiwa Spika, changamoto iliyopo Simiyu, ni maeneo yenye ukame na Wilaya zote za Simiyu zina ukame na zinapata mvua za muda mfupi. Kwa hiyo, njia ya kudumu ni ya kuyatumia maji ya Ziwa Victoria kwa ajili ya kutengeneza miradi ya umwagiliaji katika Mkoa wa Simiyu.

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. JUSTINE L. NYAMOGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga bwawa la maji katika Kata ya Nyanzwa kwa ajili ya skimu ya umwagiliaji?

Supplementary Question 4

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Wizara ya Kilimo itasambaza lini mbegu za alizeti katika Halmashauri ya Mji wa Bunda?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Robert, Mbunge wa Bunda na Wabunge wote, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mwaka jana tulisambaza jumla ya tani 2,000 za zao la alizeti za standard seed ambazo zilikumbana na changamoto na mwaka huu tutasambaza certified seed tani 2,500. Nitumie nafasi hii, kusema kwamba, halmashauri ambazo ziko tayari kushirikiana na Wizara ya Kilimo, zilete maombi na tukubaliane, mbegu hizo tunazozigawa kwa ruzuku ni namna gani fedha ile itarudi kwa sababu tutazigawa kwa ruzuku ya asilimia 50.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine ambao watakuwa tayari, tumeshafanya hivyo Mkoa wa Singida na maeneo mengine ambao watakuwa tayari hasa Ukanda wa Kati na Ukanda wa Kanda ya Ziwa ambako uzalishaji wa alizeti unafanya vizuri zaidi.