Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdulhafar Idrissa Juma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtoni

Primary Question

MHE. IDRISSA JUMA ABDUL-HAFAR aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupambana na visababishi vya maradhi yasiyoambukiza?

Supplementary Question 1

MHE. IDRISSA JUMA ABDUL-HAFAR: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Pamoja na majibu haya ya Mheshimiwa Waziri, lakini kumekuwa na ongezeko la malazi ya kisukari, malazi ya moyo pamoja na kansa kwa watoto walio chini ya miaka mitano na hata watoto kwa mujibu sheria za nchi zetu walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Je, Serikali haioni sasa iwe na utaratibu maalum wa kuhudumia kwa asilimia mia moja matibabu ya malazi yasiyoambukiza kwa watoto wote walio chini ya miaka 18? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli suala la kuhudumia watoto chini ya miaka mitano ni suala ambalo kiutaratibu wanatakiwa kupata huduma bure, bila malipo yoyote. Ni kweli kwamba kumekuwa na changamoto ya kwamba wanahitaji huduma lakini baadhi ya dawa zinakosekana. Pia, tuna mzigo mkubwa kweli wa magonjwa hayo yasiyoambukiza, ndiyo maana tunaleta Muswada wa Bima ya Afya kwa Wote wenye lengo la kusababisha sasa matatizo anayoyataja Mheshimiwa Mbunge yaweze kusuluhishwa.

Mheshimiwa Spika, ukiona uwekezaji mkubwa ambavyo umewekezwa kwenye miundombinu, vifaa tiba na tunaona mwaka huu kuna bilioni 10.7 zinaenda kutumika ni kwa ajili ya kuhakikisha wale wasiojiweza pia wanapata huduma bila malipo.

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. IDRISSA JUMA ABDUL-HAFAR aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupambana na visababishi vya maradhi yasiyoambukiza?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza ni gharama sana. Je, Serikali wanasaidia vipi wananchi kwenye gharama hizi?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwa mwaka mmoja, Serikali inatumia bilioni 670 kwa exemption yaani kwa maana na hasa asilimia kubwa ya fedha hizo zinaelekea kwenye kuwasaidia hawa wenzetu ambao wana matatizo ya magonjwa yasiyoambukiza, zinatumika hizo fedha kwa ajili ya exemption.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, Muswada wa Bima ya Afya, unakuja hapa ndani, hilo ndiyo litakuwa suluhisho na mnajua pamoja na kwamba tuna Muswada wa Bima ya Afya, Rais wetu ametenga bilioni 149.77 kwa ajili ya kuwapatia bima wale wasiojiweza. Kwa hiyo, mikakati ndiyo hiyo ya kwenda kuboresha na kuhakikisha watu wanapata huduma.