Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 26 2022-11-02

Name

Abdulhafar Idrissa Juma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtoni

Primary Question

MHE. IDRISSA JUMA ABDUL-HAFAR aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupambana na visababishi vya maradhi yasiyoambukiza?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Idrissa Juma Abdul-Hafar, Mbunge wa Jimbo la Mtoni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga shilingi milioni 725 kwa ajili ya kutekeleza Mpango Mkakati wa Tatu wa Kitaifa wa Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa Yasiyoambukiza (2021 – 2026) ambao umeainisha mikakati mahsusi ya udhibiti wa visababishi vya magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo:-

(1) Kuimarisha uratibu na ushirikishwaji wa sekta mtambuka;

(2) Kuimarisha miundombinu ya utoaji wa huduma;

(3) Kuwajengea uwezo watumishi katika kukabiliana na magonjwa yasiyoambukiza;

(4) Kuimarisha na kusimamia shughuli za utafiti; na

(5) Kuhamasisha wananchi kuhusu njia za kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza.

Njia hizi ni pamoja na kufanya mazoezi, pamoja na kuzingatia kanuni bora za lishe.