Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Kitongoji cha Cheketu Somanga Kusini watalipwa fidia kupisha ujenzi wa miundombinu ya umeme?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Katika mgogoro huu wa madai ya fidia, hivi sasa umechukua miaka mitano na jumla ya watu 63 wamehusishwa katika jambo hili: Je, Serikali ipo tayari kulipa fidia ya nyongeza kutokana na ucheleweshaji wa malipo haya?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, napenda kutaka kujua: Je, ni lini Mheshimiwa Waziri atakuwa na nafasi ya kuweza kuambatana nami twende kwa pamoja tukasuluhishe huu mgogoro? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ndulane, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nianze na la pili, tukimaliza kipindi hiki cha Bunge, tutapanga ratiba vizuri na Mheshimiwa ili tuweze kuona namna ya kumaliza jambo hili kwa pamoja kwa ajili ya kuwahudumia wananchi.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la kwanza, Serikali ipo tayari kumlipa mtu fidia kwa kadri anavyostahili kwa mujibu wa sheria. Kwa hiyo, kama nilivyosema, tutaenda pamoja na kusaidiana kutatua jambo hili, na lipatakapokwisha wale wanaostahili kulipwa fidia na kwa mazingira tuliyokuwa nayo, aidha ya ucheleweshaji au nyongeza, itafanyika kwa mujibu wa sheria.