Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 24 2022-11-02

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: -

Je, ni lini wananchi wa Kitongoji cha Cheketu Somanga Kusini watalipwa fidia kupisha ujenzi wa miundombinu ya umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Kilwa Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TANESCO inatarajia kujenga njia ya kusafirisha umeme yenye urefu wa kilomita 190 ya msongo wa kilovoti 400 kutoka Kinyerezi hadi Somanga.

Mheshimiwa Spika, Serikali tayari imelipa jumla ya Shilingi milioni 37.5 kwa wahanga 11 kati ya 13 wanaoathiriwa na mradi huu. Wahanga wawili waliobaki walitathminiwa kuwa maeneo ya Serikali ya Kijiji cha Cheketu, lakini kumekuwepo na mgogoro baina yake na wananchi. Serikali italipa malipo hayo baada ya utatuzi wa mgogoro huo.