Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA K.n.y. MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo Kikuu cha Kupooza katika Wilaya ya Mbinga?

Supplementary Question 1

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ninaishukuru Serikali kwa majibu mazuri, nina swali moja la nyongeza lenye sehemeu (A) na (B).

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa lane iliyopo sasa ni hiyo ambayo inayotumika Songea, inatumika Mbinga pia inatumika Nyasa. Kwa kuwa kuna ongezeko kubwa sana la utumiaji wa umeme kutokana na uchimbaji mkubwa wa makaa ya mawe pale Mbinga, viwanda vikubwa vya kubangua kahawa, viwanda vya kusaga sembe na viwanda vya maji ni vingi hali inayopelekea umeme kuwa wa low voltage au kukatikakatika.

Je, Serikali iko tayari kurudisha mpango wake nyuma badala ya mwaka 2024/2025 uwe 2023/2024 ili kuwafanya wananchi nao wapate nafasi ya kutumia umeme ambao sasa haukatikikatiki.

Mheshimiwa Spika, ikiwa hili haliwezekani, je, Serikali itaisaidiaje Mbinga kuondokana na hali hii ya kukatika katika kwa umeme?(Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza lililoulizwa na Mheshimiwa Benaya Kapinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nikweli kwamba Mkoa wa Ruvuma umekuwa na changamoto ya maeneo kuwa na matatizo ya low voltage, na kwa sasa kwenye bajeti ya mwaka huu, kama tulivyosema tumeiweka Mbinga, kuna line ya kujengwa inayotoka Songea kwenda Tunduru ambayo ina kilometa kama 211. Serikali ilifanya uhakiki wa matatizo na ikagundua kwamba hapo kuna changamoto kubwa zaidi, na wako wale wenye changamoto kidogo na ambao hawana changamoto zaidi. Kwa hiyo eneo la Mbinga limewekwa kwenye wale wasiokuwa na changamoto sana kama hao wengine.

Mheshimiwa Spika, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kuifanyia marekebisho na matengenezo ya mara kwa mara hii line ya kutoka Songea kwenda Mbinga na tuone uwezekano wa kuivuta mapema kabla ya ule muda uliopangwa kulingana na bajeti itakavyokuwa imewekwa.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA K.n.y. MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo Kikuu cha Kupooza katika Wilaya ya Mbinga?

Supplementary Question 2

MHE. ENG. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Wilaya ya Hanang tunachangamoto kubwa sana ya umeme kukatika mara kwa mara, na suluhu ya tatizo hili ni kujengwa kwa kituo cha kupooza umeme pale Mogitu. Serikali iliahidi kutoa zaidi ya shilingi bilioni mbili ili ujenzi huo ufanyike.

Je ujenzi huo utaanza lini?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hhayuma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyotangulia kujibu kwenye maswali mengine, Serikali imefanya utafiti na kubaini maeneo yanayohitaji kujengwa vituo vya kupooza umeme kwa ajili ya kuhakikisha huduma inawafikia wananchi, na eneo hilo ni mojawapo kati ya maeneo ambayo yametengewa na muda utakapofika huduma hiyo itatekelezwa kwenye jimbo lake.