Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 20 2022-11-01

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA K.n.y. MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo Kikuu cha Kupooza katika Wilaya ya Mbinga?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jonas William Mbunda, Mbunge wa Mbinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza kutekeleza mpango wa kuimarisha Gridi ya Taifa uliopewa jina la ‘Gridi Imara’ kwa kujenga miundombinu ya usafirishaji na usambazaji umeme pamoja na vituo vya kupooza na kudhibiti umeme.

Mheshimiwa Spika, mpango huu una miradi zaidi ya 40 na utatekelezwa ndani ya miaka Mitano (5) kuanzia mwaka huu wa fedha 2022/2023 ambapo Serikali imekwishatenga jumla ya Shilingi Bilioni 500 kwa ajili ya kugharamia miradi yenye vipaumbele vya kwanza.

Mheshimiwa Spika, mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovolts 220 yenye urefu wa kilometa 93.5 kutoka Songea hadi Mbinga na ujenzi wa kituo cha kupooza umeme cha ukubwa wa Megawatt Mbili mara 30, kV 220 kwenda 33 utatekelezwa kuanzia mwaka wa fedha 2024/2025 na unatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka mmoja na nusu tangu utakapoanza. (Makofi)