Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, ni lini Miradi ya maji Halmashauri ya Msalala itaanza kutekelezwa baada ya Serikali kutenga Shilingi bilioni 4.8 kwa ajili ya miradi hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, maswali yangu mawili ya nyongeza. Swali langu la kwanza: Mchakato wa ununuzi wa mabomba ambao ulikuwa unasimamiwa na Wizara na baadaye kurudishwa mkoani, sasa ni lini Serikali itaharakisha mchakato huo wa manunuzi ili wakazi wa Busangi waweze kutumia maji katika eneo hilo?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili: Mkandarasi anayejenga mradi unaotoka Mangu – Ilogi bado ameendelea kuchelewesha malipo ya wafanyakazi: Ni lini Serikali itamhimiza mkandarasi huyo ili aweze kuwalipa watumishi wake fedha hizo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maji imeangalia namna ya kutatua tatizo la maji hasa maeneo ya vijijini. Tumeanzisha Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) na Bunge lako Tukufu tunalishukuru. Tunapoanzisha taasisi yoyote tunakuwa na mikakati. Tumeweka kwa ajili ya manunuzi wizarani, sasa yameshuka mikoani. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Wizara yetu itaendelea kufanya marekebisho ili kuhakikisha utekelezaji wa miradi ya maji inafanyika kwa urahisi zaidi.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, malipo ambayo mkandarasi amekuwa akichelewesha kulipa watumishi wanaofanya kazi, namwomba Mheshimiwa Mbunge, kwa kuwa baadaye saa 7.00 Bunge litakuwa limeasitishwa, tukutane ili tuzungumze na Mkandarasi moja kwa moja kwa ajili ya malipo ya watumishi wake. Ahsante sana.

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, ni lini Miradi ya maji Halmashauri ya Msalala itaanza kutekelezwa baada ya Serikali kutenga Shilingi bilioni 4.8 kwa ajili ya miradi hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tarehe 6/6/2022 Serikali yetu iliingia mkataba wa ujenzi wa mradi wa maji kutoka Mto Ruvuma kuja Mji wa Mangaka, miezi minne imefika. Naomba kupata kauli ya Serikali, ni lini mkandarasi atakuwa site ili kutekeleza mradi huo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru na nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, kweli eneo la Nanyumbu ni eneo ambalo limekuwa na changamoto sana ya maji. Tumesaini mradi huu tarehe 6/6/2022 kama alivyoeleza, kwa sasa tuna-process advance payment kwa Mkandarasi ili kuhakikisha kwamba anakwenda kutekeleza mradi kwa haraka na wananchi wake waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, ni lini Miradi ya maji Halmashauri ya Msalala itaanza kutekelezwa baada ya Serikali kutenga Shilingi bilioni 4.8 kwa ajili ya miradi hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali ilikubali kutoa Shilingi milioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa tenki la kuchujia maji: Je, ni lini pesa hiyo itatolewa ili ujenzi huo uanze?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ni kweli tulitoa ahadi na ahadi ni deni. Nimwahidi Mheshimiwa Mbunge ndani ya mwezi huu tutaoa pesa kwa sababu tumeshapokea pesa za Mfuko wa Maji na tutawapa kipaumbele katika Jimbo lake.