Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 1 Water and Irrigation Wizara ya Maji 9 2022-11-01

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: -

Je, ni lini Miradi ya maji Halmashauri ya Msalala itaanza kutekelezwa baada ya Serikali kutenga Shilingi bilioni 4.8 kwa ajili ya miradi hiyo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi Mbunge wa Jimbo la Msalala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji katika Halmashauri ya Msalala. Katika mwaka wa fedha 2021/2022, jumla ya miradi mitano ilikamilika. Katika mwaka 2022/2023, Serikali inaendelea na ujenzi wa miradi 12 ambapo miradi miwili imekamilika na miradi 10 ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Mheshimiwa Spika, aidha, utekelezaji wa mradi wa maji wa Mhangu – Ilogi awamu ya kwanza umekamilika na tayari unatoa huduma katika Kijiji cha Ilogi. Utekelezaji wa awamu ya pili unaendelea na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Desemba, 2022. Mradi huu ukikamilika utakuwa na bomba lenye urefu wa kilomita 37.5, matenki manne yenye jumla ya ujazo wa lita 440,000 na vituo 32 na kunufaisha wananchi wapatao 24,436.