Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kufanya utafiti kuhusu hali ya biashara na uchumi wa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, nataka tu kujua Serikali ilipofanya tafiti imegundua ni kwanini wafanyabiashara wengi hasa wadogo wadogo wanafunga biashara zao hivyo kupelekea hali ya uchumi kudolora hususan Mkoani kwetu Mtwara?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, nataka tu kujua mkakati wa Serikali ukoje kuhakikisha unawaunganisha wananchi wa mkoa wa Mtwara na fursa ya masoko katika nchi ya Comoro?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Tunza Issa Malapo Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema, moja ya mikakati tunayoifanya ni kuhakikisha tunafanya tafiti mbalimbali. Moja kwa kuwashirikisha taasisi za umma lakini pia na wadau wa maendeleo ambao wanafanya tafiti hizo kuhusiana na hali ya uchumi lakini pia na namna ya kufanya biashara nchini.

Mheshimiwa Spika, moja ya matokeo ambayo yanaonesha pamoja na kwamba kuna udolora wa wafanyabiashara wadogo lakini ni changamoto za maeneo. Ndiyo maana Serikali imekuja na mpango wa kuwapanga katika maeneo mahususi ili wawe na maeneo ambayo ni mazuri na rafiki kwa wafanyabiashara wadogo wadogo ambao mara nyingine wakikaa maeneo ambayo si rafiki kunakuwa na ile changamoto zak ukimbizwa na baadhi ya mgambo na taasisi zingine ambazo wafanyabiashara wadogo wanakuwa wamevamia na kufanya biashara zao katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili, ni kweli tunaendelea kutafuta, moja ya changamoto yao ya mitaji ambayo tunaifanyia kazi ili wafanyabiashara wadogo wadogo waweze kupata mitaji kwa njia rahisi. Lakini zaidi pia tutaendelea kuwatafutia maeneo ya kufanyia biashara katika Mkoa wa Mtwara kama ulivyosema lakini pia na maeneo mengine nchini, ili wafanyabiashara wadogo kwanza wapate mitaji lakini pili wawe na maeneo mahususi ya kufanya biashara bila kusumbuliwa.