Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 1 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 5 2022-11-01

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kufanya utafiti kuhusu hali ya biashara na uchumi wa wananchi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Issa Malapo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeweka utaratibu wa kupata matokeo ya tafiti zinazolenga kuboresha biashara na uchumi wa wananchi pamoja na kuwaunganisha wananchi na fursa za masoko kupitia maonesho ya mifuko na programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi.

Mheshimiwa Spika, aidha, pamoja na hiyo mikakati mingine ni kutoa tuzo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya tafiti bora kwenye masuala ya uchumi na biashara.