Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdullah Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mahonda

Primary Question

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI aliuliza: - Je, Serikali imechukua hatua gani kutatua changamoto zinazoelezwa za ukiritimba zilizopelekea Kampuni ya Uber kusitisha huduma zake nchini Tanzania?

Supplementary Question 1

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana pamoja na majawabu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Kwa kuwa Uber inachangia kwa kiasi kikubwa sana ajira nyingi za vijana; je, Serikali haioni kwamba ajira ya vijana ina mchango chanya zaidi kushinda hizi tozo ndogo ambazo Serikali imeziweka?

Swali la pili; kwa kuwa Uber ni kampuni ya teknolojia na siyo kampuni ya usafiri, Uber ulimwengu mzima haina gari hata moja, inawezesha watu wenye magari kuweza kufanya biashara ya usafiri wa taxi kirahisi na kwa kuhuda nafuu.

Je, taasisi ya LATRA (Mdhibiti wa Magari ya Ardhini) ni taasisi sahihi kufanya majadiliano na kampuni ya Uber? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante napenda kujibu mawali mawili kwa pamoja ya Mheshimiwa Abdullah Ali Mwinyi, Mbunge wa Mahonda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba Uber pamoja na mashirika mengine ambayo yalikuwa yanatoa huduma za taxi mtandao yanatoa ajira kubwa kwa vijana, lakini pia yanatoa huduma kwa wasafiri. Kilichopelekea kusitisha huduma kwa kampuni hii ya Uber na Bolt ilikuwa ni baada ya LATRA kuona uwezekano wa wao kupunguza kamisheni ambapo walikuwa wanatoa zaidi ya asilimia 25 na kukawa kuna malalamiko ya wamiliki wa taxi ambapo waliona kamisheni ile sasa hawafanyi kazi vizuri ndiyo maana wakasimama.

Kwa hiyo ilikuwa ni kuona ni namna gani wamiliki wa taxi watapata faida lakini wamiliki wa haya makampuni ya taxi mtandao watapata faida, lakini pia bila kumuumiza abiria.

Mheshimiwa Spika, tarehe 5 mpaka 8 Septemba, 2022 LATRA, wamiliki wa hizi taxi pamoja na wasafirishaji wengine wamekaa na wamekubaliana kupata muafaka na kabla ya mwisho wa mwezi huu Serikali itatoa taarifa maana kumekuwa na mazungumzo mazuri ili kuwa na win win situation kwa msafiri, mwenye taxi lakini na kampuni hizi ambazo zinasimamia huu usafiri wa taxi mtandao, ahsante.