Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 20 2022-09-13

Name

Abdullah Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mahonda

Primary Question

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI aliuliza: -

Je, Serikali imechukua hatua gani kutatua changamoto zinazoelezwa za ukiritimba zilizopelekea Kampuni ya Uber kusitisha huduma zake nchini Tanzania?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abdullah Ali Mwinyi, Mbunge wa Mahonda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) ilianza kudhibiti huduma za taxi mtandao mwezi Mei, 2020 kwa kutumia Sheria ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini Na. 3 ya mwaka 2019 pamoja na kanuni zake.

Mheshimiwa Spika, baada ya LATRA kuanza kudhibiti eneo hili kisheria, iliweka viwango vya tozo kwa huduma za taxi ili kupunguza migogoro kati ya madereva na wamiliki wa mifumo ya taxi ambao ni pamoja na Kampuni ya Uber. Kutokana na hatua ya LATRA kuweka tozo katika huduma za taxi mtandao, Kampuni ya Uber iliamua kusitisha kutoa baadhi ya huduma hapa nchini mwezi Aprili, 2022.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia LATRA inaendelea na mazungumzo na Kampuni ya Uber kwa lengo la kuhakikisha inarejesha huduma za taxi mtandao. Ahsante.