Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Ali Omar

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Wete

Primary Question

MHE. OMAR ALI OMAR aliuliza: - Je, wanafunzi wangapi kutoka Zanzibar wamepata mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka 2020/2021?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ALI OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba niulize swali moja la nyongeza.

Kati ya wanafunzi 1,492 ni wanafunzi wangapi wenye mahitaji maalum ambao walipatiwa mkopo huo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda sasa kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Omar Ali Omar Mbunge wa Wetu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, miongoni mwa vigezo ambavyo vinatumiwa na Bodi ya Mikopo yetu ya Elimu ya Juu ni pamoja na ulemavu, kwa maana ya wenzetu wenye mahitaji maalum pamoja ya uyatima. Kwa hiyo nitatoa takwimu tu za jumla za wenzetu hao kwenye makundi hayo kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Spika, kwa kipindi cha mwaka 2021 wanufaika wote wa Bodi ya Mikopo walikuwa ni 149,389; kwa upande wa Zanzibar wale waliokuwa na mahitaji maalum walikuwa ni 100; na mwaka 2021/2022 yaani mwaka huu tunaoendelea nao jumla ya wanufaika wote ni 177,892 na wale wenye mahitaji maalum kwa upande wa Zanzibar peke yake walikuwa ni 181. Nakushukuru.

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OMAR ALI OMAR aliuliza: - Je, wanafunzi wangapi kutoka Zanzibar wamepata mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka 2020/2021?

Supplementary Question 2

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Spika, ni kwa nini sasa Serikali isione haja ya kushirikisha taasisi binafsi za fedha ili ziweze kutanua wigo wa kupata fedha zaidi kwa ajili ya kutoa mikopo na yenyewe ibaki ku-regulate tu?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Nusrat Hanje, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge hivi sasa tunaendelea na mazungumzo na taasisi mbalimbali za fedha, lakini katika bajeti yetu ya mwaka 2022/2023 tayari wenzetu wa NMB wameweza kuongeza bajeti yetu ya mikopo kwa ajili ya vijana wetu wa elimu ya juu pamoja na elimu ya kati zaidi ya shilingi bilioni 200. Kwa hiyo kama Serikali tunalifanya hilo na tutaendelea kulifanya.