Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juliana Didas Masaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. MASABURI aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kufanya ukaguzi wa kudhibiti uingizaji na utengenezaji wa vipodozi fake nchini?

Supplementary Question 1

MHE. JULIANA D. MASABURI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu hayo ya Serikali ambayo bado hayaridhishi napenda kuiuliza Serikali; tangu nimeandika hili swali najua kuna shirika la TBS najua kuna Tume ya Ushindani; lakini bidhaa fake hasa vipodozi, vyakula vimezidi kuzalishwa nchini na kuingizwa kwa kasi ya juu. Naomba majibu sahihi ya Serikali nini wanapanga kudhibiti bidhaa fake? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juliana Didas Masaburi Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli changamoto ya bidhaa fake ni ya kudumu. Na kwa namna ambavyo tunajua lazima tuendelee kudhibiti. Serikali inaendelea kufanya juhudi mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, mojawapo ya changamoto tuliyonayo ni upungufu wa watumishi katika taasisi zetu hizi za TBS na FCC. Hata hivyo tunaendelea kuboresha ili kupata watumishi wa kutosha. vilevile tunaweka nguvu au mkazo kwenye elimu kwa umma, kwasababu bidhaa fake au bidhaa hizo au vipodozi hivi vinavyoingizwa ni kwasababu ya mahitaji ambayo Watanzania wanahitaji. Kwa hiyo, tukiwapa elimu sahihi maana yake vitakosa soko au uhitaji wa bidhaa hizo. Kwa hiyo tutaendelea kutoa elimu pamoja kuimarisha zaidi kwa kuhakikisha tunapata watumishi wa kutosha ili wasaidie kudhibiti mianya ambayo inatumika kuingiza bidhaa hivi fake na vipodozi ambavyo vinakosa sifa za kutumika kwa ajili ya kudhibiti soko la Tanzania.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. JULIANA D. MASABURI aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kufanya ukaguzi wa kudhibiti uingizaji na utengenezaji wa vipodozi fake nchini?

Supplementary Question 2

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Mheshimiwa Spika, kwenye swali la msingi la vipodozi fake kweli ni janga la Kitaifa.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kwamba vipodozi vinapendezesha (beautifying) lakini kazi kubwa ya vipodozi ni za kiafya katika ngozi na mwili. Swali langu la msingi ni kwamba, ni lini Serikali itahamisha bidhaa za vipodozi kutoka Wizara ya Uwekezaji Viwanda na Biashara kwenda Wizara ya Afya ambapo kuna wataalam wa vipodozi hivyo ili tuweze kulinda afya ya jamii? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Florent Kyombo (Mb) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika ni kweli vipodozi ni sehemu ya bidhaa ambayo ipo kwenye kundi la dawa. Sasa, kwasababu ni ushauri Serikali tunalichukua ili tuweze kuona namna gani tutaliweka hili suala liweze kutumiwa kwenye sehemu sahihi kama sio Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara, nakushukuru.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. MASABURI aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kufanya ukaguzi wa kudhibiti uingizaji na utengenezaji wa vipodozi fake nchini?

Supplementary Question 3

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwakuwa tumekuwa tukishuhudia kila mara vitu hivyo au vipondozi hivyo, vyakula hivyo vikichomwa katika maghara na kwa gharama kubwa sana. Je, ni nani anayegharamia, kwasababu yule aliyenyang’anywa tayari ameshafilisika?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shally Raymond (Mb) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli, kwamba kwa utaratibu anayetakiwa kugharamia uharibifu wa bidhaa hizo fake au vipodozi ni yule ambaye ameingiza, kwa maana ya aliyekiuka sheria ya uingizaji wa bidhaa, kwasababu zidhaa zote ambazo zinaruhusiwa kuuzwa katika masoko ya Tanzania hasa vipodozi lazima viwe vimesajiliwa. Kwamba, kama vimeingizwa kinyume na sheria hiyo yeye ndiye atakayetakiwa kulipa ili kuhakikisha anafidia gharama hizo za kuharibu vipodozi, nashukuru.