Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 30 2022-09-14

Name

Juliana Didas Masaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. MASABURI aliuliza: -

Je, Serikali imejipangaje kufanya ukaguzi wa kudhibiti uingizaji na utengenezaji wa vipodozi fake nchini?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara napenda kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Didas Masaburi, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Shirika la Viwango Tanzania yaani TBS imeendelea kudhibiti uingizaji na utengenezaji wa vipodozi visivyokidhi viwango vya ubora kwa mujibu wa Sheria ya Viwango Na. 2 ya Mwaka 2009 na Sheria ya Fedha Na. 8 ya Mwaka 2019. Pia Serikali imeendelea kudhibiti bidhaa fake kupitia Tume ya Ushindani (FCC) kwa mujibu wa Sheria ya Ushindani Na. 8 ya Mwaka 2003.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.