Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SYLVESTRY F. KOKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuijenga kwa kiwango cha lami njia nane barabara ya Dar es Salaam hadi Morogoro?

Supplementary Question 1

MHE. SYLVESTRY F. KOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara ya TAMCO - Mapinga - Kibaha inayojengwa kiwango cha lami imekuwa inasuasua kwa muda mrefu, lakini pamoja na hilo wale wananchi waliopisha ujenzi wa barabara hii hawajalipwa fidia hadi leo kwa maana ya wananchi wa kata ya Tangini na Pangani. Je, ni lini wananchi hawa watalipwa fidia kama kwa mujibu wa sheria ulivyo?

Swali la pili barabara ya zamani kwa maana ya Dar es Salaam - Morogoro inayoanzia sasa Picha ya Ndege mpaka Mlandizi ni barabara ambayo ni kimbilio la wasafiri na wasafirishaji hasa barabara hii kubwa inapopata tatizo la ajali na kufunga barabara.

Sasa kwa umuhimu huo ni lini Serikali itaweka nguvu kurekebisha barabara hii ili iweze kupitika na kusaidia kutokuondoa msongamano wa barabara kubwa wakati kunapokuwa na ajali?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Sylvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara ya TAMCO - Mapinga kumekuwa na ujenzi wa kusuasua na pia baadhi ya watu hawakulipwa fidia. Naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inalifahamu jambo hili na inalifanyia kazi kuhakikisha kwamba hawa watu wanalipwa na ujenzi huu unakamilika kwa muda kwa hii barabara ya TAMCO - Mapinga ambayo ni barabara muhimu sana.

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu barabara aliyosema ambayo itakuwa ni msaada mkubwa sana kwa ajili ya kusaidia panapotokea changamoto kwenye eneo hili la picha ya ndege naomba nichukue suala la Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali kwa maana ya Wizara kupitia TANROADS tutalifanyia kazi kuhakikisha kwamba barabara hii inaboreshwa iwe ni msaada pale ambapo barabara kuu inapopata changamoto inatusaidia kuhakikisha kwamba hatupati changamoto kubwa kwa maana ya kukwama. Ahsante.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SYLVESTRY F. KOKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuijenga kwa kiwango cha lami njia nane barabara ya Dar es Salaam hadi Morogoro?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Bujela -Masukulu na kuekelea Matebe na kutokea Kyela ni barabara muhimu sana kiuchumi kwa maana kokoa, chai inatoka maeneo hayo. Serikali haioni umuhimu wa kuijenga angalau kwa lami ili kuweza kusaidia uchumi wa wananchi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba barabara zote tungependa tuzijenge kwa kiwango cha lami, lakini hatuwezi kuzijenga zote kwa wakati mmoja kwa sababu ya ufinyu wa bajeti. Kwa hiyo, tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali italichukua na ni mpango kwamba hizi barabara ikiwemo na hii barabara aliyoitaja kujengwa kwa kiwango cha lami, lakini kikubwa itategemea tu na uwezo wa bajeti ya Serikali. Ahsante.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SYLVESTRY F. KOKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuijenga kwa kiwango cha lami njia nane barabara ya Dar es Salaam hadi Morogoro?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa Serikali ina mpango wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Ndala kwenda Mwawaza kuliko na Hospitali ya Rufaa. Je, ni lini itaanza kutekeleza mpango huo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christina Mnzava, Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii itaanza kujengwa pale tu ambapo fedha itapatikana kwa ajili ya kuanza ujenzi wa hiyo barabara muhimu. Ahsante.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SYLVESTRY F. KOKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuijenga kwa kiwango cha lami njia nane barabara ya Dar es Salaam hadi Morogoro?

Supplementary Question 4

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante nashukuru kwa kunipa nafasi.

Ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kutoka Namanyere - Kilando mpaka Kipili kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bupe Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Rukwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Namanyere hadi Kipili ambayo inaenda bandarini ni barabara muhimu na barabara hii iko kwenye usanifu, kwa hiyo baada ya kukamilisha usanifu wa kina Serikali itatafuta fedha ili ianze kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. SYLVESTRY F. KOKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuijenga kwa kiwango cha lami njia nane barabara ya Dar es Salaam hadi Morogoro?

Supplementary Question 5

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali.

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi naomba kuuliza barabara ya kutoka Masumbwe kwenda Geita Makao Makuu ya mkoa ni lini itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nicodemas Maganga, Mbunge wa Mbogwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Masumbwe kwenda Geita imeshafanyiwa usanifu wa kina na sasa Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. SYLVESTRY F. KOKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuijenga kwa kiwango cha lami njia nane barabara ya Dar es Salaam hadi Morogoro?

Supplementary Question 6

MHE. BONNAH L. KAMOLI: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri ni lini barabara ya Bonyokwa - Kimara itaanza kujengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah, Mbunge wa Segerea kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba amefika mara kadhaa Wizarani na Mheshimiwa Waziri pamoja na TANROADS Mkoa wa Dar es Salaam wamemuahidi na mimi nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hiyo kutoka Bonyokwa kwenda Kimara ipo kwenye mpango kwa ajili ya kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.