Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 26 2022-09-14

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SYLVESTRY F. KOKA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuijenga kwa kiwango cha lami njia nane barabara ya Dar es Salaam hadi Morogoro?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa la Mheshimiwa Sylvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imetangaza zabuni kwa ajili ya Expression of Interest kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya njia nne kutoka Kibaha – Mlandizi – Chalinze hadi Morogoro yenye urefu wa kilometa 205 kwa utaratibu wa Engineering, Procurement, Construct and Finance (EPC + F). Gharama za ujenzi wake zitatolewa na Serikali au na sekta binafsi (PPP) kwa utaratibu wa Jenga, Endesha, Rudisha (Build Operate and Transfer) ambapo sekta binafsi itajenga barabara hii kwa fedha zake na kuiendesha hadi pale itakaporejesha fedha zake kupitia tozo za magari. Ahsante.