Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya sintofahamu ya utaratibu wa kuwapata wanafunzi wanaorudishwa masomoni?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa fursa hii pamoja na mwongozo uliotolewa na Serikali lakini bado utekelezaji wake ni mdogo kwenye halmashauri zetu zote.

Je, Serikali ina mkakati wa kusimamia mwongozo huu?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, je, Serikali haioni haja sasa ya kutunga sheria ya kuhusu jambo ili basi kuwanusuru wanafunzi wetu? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zaytun Seif Swai, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha kwamba huu mwongozo unasimamiwa na jukumu letu sisi kama Ofisi ya Rais-TAMISEMI, ni kufuatatilia utekelezaji wa mwongozo huu na tathmini yake. Kwa hiyo, niseme tu tutarudi tena tutawaagiza Maafisa Elimu kuhakikisha kwamba agizo la Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu la wanafunzi wote waliokatishwa masomo wanarudi shuleni linatekelezwa kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Spika, suala la pili, kuhusu sheria, tumelipokea wazo hili ni jema, na sisi kama Serikali tukishirikiana na Bunge tutafanya mchakato kuhakikisha kwamba sheria hiyo inaletwa Bungeni ili tuweze kuwalinda Watoto hao ambao wameacha shule. Ahsante sana.