Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, ni programu zipi zinatekelezwa kuvuna maji ya mvua na asilimia ngapi ya Wananchi hutumia huduma hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Je, ni lini sharti litawekwa sasa baada ya kutoa mwongozo huo (Building Regulations) ya majengo yote ya Serikali na hata ya watu binafsi kuwa na makingamaji ili waweze kuihifadhi hayo maji ya mvua?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili: Kwa kuwa maji hayo yanaharibu sana barabara wakati wa masika, hasa maeneo ya mlimani kama ya Wilaya zote za Mkoa wa Kilimanjaro na yanaosha kabisa ile changarawe kwenye barabara: Ni lini mitaro mikubwa itajengwa katika barabara hizo ili iwe salama? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa na nzuri ambayo anaifanya, lakini kubwa ambalo nataka nimhakikishie kupitia Wizara yetu ya maji tumeshatoa maelekezo na tumekubaliana kwamba mvua isiwe maafa, mvua iwe fursa. Kwa hiyo, moja ya mkakati wetu ni kuwa na ushirikiano na Wizara nyingine, kwa maana ya Wizara ya TAMISEMI. Mwananchi kule anapotaka kujenga nyumba yake, basi uwekwe utaratibu namna gani anaweza kuvuna maji ya mvua ili aweze kuondokana na matatizo ama changamoto ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kikubwa, Wizara ya Maji itashirikiana na Wizara nyingine ikiwemo Wizara ya TAMISEMI ili kuhakikisha wananchi wetu nyumba wanazojenga wanaweka miundombinu ya uvunaji wa mvua.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lingine, tumeona baadhi ya maeneo mbalimbali mvua inaponyesha inaleta maafa na kuleta athari mbalimbali. Maelekezo ya Mheshimiwa Rais katika Wizara yetu ya Maji ni juu ya ujenzi wa mabwawa ili kuhakikisha kwamba tunavuna maji na kwa kushirikiana na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kujenga miundombinu ili mvua zinaponyesha zisilete athari na badala yake iwe fursa kwa wananchi wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)