Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 65 2022-09-16

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: -

Je, ni programu zipi zinatekelezwa kuvuna maji ya mvua na asilimia ngapi ya Wananchi hutumia huduma hiyo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shally Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilibuni Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDP) inayotekelezwa nchini kote kuanzia mwaka 2006 hadi 2025. Programu hiyo inatekelezwa kupitia Programu ndogo tatu ambapo pamoja na mambo mengine, programu hizo zinazingatia uvunaji maji ya mvua kwa kuelekeza ujenzi wa mabwawa makubwa, ya kati na madogo na pia, uvunaji wa maji ya mvua kwa kutumia mapaa ya nyumba.

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia programu hizo, mabwawa yamejengwa na kukarabatiwa kwenye maeneo mbalimbali nchini na katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali inaendelea na ujenzi na ukarabati wa mabwawa ya ukubwa wa kati na madogo katika wilaya 16, ujenzi wa mabwawa ya kimkakati ya Farkwa na Kidunda na usanifu wa ujenzi wa mabwawa katika Wilaya 24. Aidha, Serikali ilitoa mwongozo wa Uvunaji wa Maji ya Mvua kupitia mapaa ya nyumba kwa watu binafsi na taasisi za Umma na kwa sasa miundombinu hiyo inaonekana katika maeneo mbalimbali nchini. Serikali itatafiti kufahamu ukubwa wa matumizi ya teknolojia hiyo nchini.