Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza: - Je, Serikali ipo tayari kuanzisha shule maalum kikanda ili kusaidia watoto walioathirika na ukatili wa kijinsia?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, asante sana kwa kunipa nafasi ili niulize maswali madogo mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa ukatili huo upo nchi nzima, kwa nini vituo hivi vimejengwa katika mikoa miwili tu yaani Dodoma vituo 20, Dar es Salaam vituo 10, ilhali changamoto hii ipo nchi nzima ikiwepo Mkoa wetu wa Iringa?

Mheshimiwa Naibu Spika, je, Wizara hii sasa haioni haja ya kushirikiana a Wizara ya Elimu ili kuwa na shule maalum zitakazotoa msaada kwa watoto walioathirika na ukatili huo kama ilivyofanyika katika programu ya MEMKWA?

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ritta Kabati Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu hivi vituo 30 vilivyoanzishwa vilikuwa ni vituo vya awali vya majaribio ili kutuwezesha kuona jinsi mfumo unavyofanya kazi. Kwa sasa tumeshaona na tayaru tuko kwenye maandalizi ya mwongozo wa jinsi ya kuvianzisha na kuviendesha nchi nzima, katika mikoa yote. Tunatarajia mapema mwakani mwongozo ukamilike ili tuende nchi nzima.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili kuhusu kuufanya mfumo tuwe kama mfumo wa MEMKWA katika suala zima la kuwafundisha hawa watoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, mfumo uliopo unafanya kazi vizuri kiasi kwamba mtoto anapokutwa na matatizo anapata huduma za kisheria, kisaikolojia, kiafya, chakula na tunamrejesha kuendelea na maisha. Ikitokea sasa kuna tatizo lingine linalozuia asiendelee vizuri tunawapeleka kwenye nyumba salama makao ya watoto na hapo tunaungana na Wizara ya Elimu kutafuta aendelee shule gani tofauti na ile ya awali. Hivyo basi, tumepokea maoni kama itabidi iwe hivyo tutajadili na Wizara ya Elimu kwa nyakati zijazo tuone jinsi ya kufanya, lakini sasa hivi mfumo unafanya kazi vizuri.