Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Kahama – Nyangh’wale – Busisi hadi Sengerema itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; kwa kuwa barabara ile inaunganisha na barabara ya Sengerema- Ngoma, je ni lini itafanyiwa usanifu?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, barabara ya Sengerema- Kamanga imeshafanyiwa usanifu, leo ni miaka mitatu; je, ni lini itajengwa kwa lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tabasam Mbunge wa Sengerema kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Sengerema- Ngoma haijafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na ipo kwenye Ilani. Tumemwagiza meneja wa Mkoa wa Mwanza aweze kuangalia kama kutapatikana fedha yoyote kwenye fedha ya maendeleo basi aielekeze kufanya usanifu wa barabara hii kwa sababu ni barabara fupi sana. Na barabara ya Sengerema – Kamanga Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Kahama – Nyangh’wale – Busisi hadi Sengerema itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Utegi-Shirati mpaka Kilongwe ni barabara ya kimkakati inayounganisha nchi mbili kati ya Tanzania pamoja na Kenya kwa kupitia Wilaya ya Rorya. Na kwa kuwa tayari upembuzi yakinifu wa barabara hii umeshakamilika nilitaka nijue ni lini sasa barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chege, Mbunge wa Rorya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli barabara hii ni muhimu kwa sababu inaunganisha Tanzania na Kenya. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Kahama – Nyangh’wale – Busisi hadi Sengerema itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujua barabara yetu ya Ubena Zomozi-Ngerengere ya kilometa 10?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Taletale Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Mbena Zomozi imeshapata kibali kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami hizo kilomita alizozisema. Ahsante.