Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 4 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 61 2022-09-16

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza: -

Je, ni lini barabara ya Kahama – Nyangh’wale – Busisi hadi Sengerema itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu Swali la Mheshimiwa Hussein Nassor Amar, Mbunge wa Nyangh’wale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Katika mwaka wa fedha 2022/23 Serikali imetenga kiasi cha Shilingi milioni 300 kwa ajili ya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ikiwa ni maandalizi kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Kahama – Nyangh’wale – Busisi hadi Sengerema yenye urefu wa kilometa 163. Baada ya kazi hiyo kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi. Ahsante.