Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO K.n.y. MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga uwanja wa ndege wa Omukajunguti?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kunipatia fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nishukuru kwa majibu ya Serikali yenye kutia moyo. Lakini tungependa kujua kutokana na wingi wa abiria katika Mkoa wa Kagera.

Je, ni lini shughuli ya kuwalipa fidia wakazi wa eneo lile kama mchakato wa kuanza ujenzi wa uwanja wa kimataifa wa Omukajunguti itafanyika?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kutokana na wingi wa abiria unaokabili Uwanja wa Ndege wa Bukoba, je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha miruko zaidi ya mmoja ili kukabiliana na mahitaji ya usafiri wa anga kwa wakazi wa Mkoa wa Kagera?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba kuna timu iliundwa na mwezi uliopita ilienda kutembelea eneo la Uwanja wa Omukajunguti ili kujiridhisha kama una uvamizi kiasi gani, ikiwa ni maandalizi ya kuanza kulipa fidia. Kwa hiyo taarifa itakavyotoka taraibu zitaanza ili wananchi waweze kulipwa na maandalizi ya ujenzi wa uwanja huu uanze.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa suala la pili linalohusu miruko, suala la ndege ni biashara pia ni huduma. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Shirika la Air Tanzania wamesikia na watafanya tathmini kuona kama kuna umuhimu wa kuongeza safari zingine.

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO K.n.y. MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga uwanja wa ndege wa Omukajunguti?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Naibu Spika, asante kwa kunipatia nafasi.

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa upanuzi wa uwanja wa Mkoa wa Kigoma?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Kibondo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wa Mkoa wa Kigoma kwamba nyaraka za zabuni kwa sasa ziko kwa Mwanasheria Mkuu kwa ajili ya vetting ili kazi ya upanuzi wa uwanja huo zianze. Ahsante.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO K.n.y. MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga uwanja wa ndege wa Omukajunguti?

Supplementary Question 3

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Ifakara ni mji unaokuwa kwa kasi sana na uwanja wake wa ndege ni dhoofu. Ni lini Serikali itakarabati Uwanja wa Ndege wa Ifakara ili ndege kubwa ziweze kutua?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asenga Mbunge wa Kilombero kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tulichukue. Hata hivyo niwaagize watu wa TAA na TANROADS wautembelee uwanja huo kwa ajili ya kuufanyia ukarabati. Ahsante.