Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, Serikali ina taarifa juu ya madini yanayopatikana Kakonko na wananchi wananufaikaje nayo?

Supplementary Question 1

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Aidha, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa madini hayo katika Wilaya yetu ya Kakonko ni uthibitisho wa utajiri na hazina kubwa ya madini katika Wilaya yetu.

Je, ni lini sasa Serikali itaanza uchimbaji mkubwa ili wananchi na Serikali iweze kufaidi kwa kiwango kikubwa zaidi? (Makofi)

Swali la pili, Serikali ina mpango gani sasa wa kuwawezesha wananchi na wachimbaji wadogo wadogo mtaji ili uchimbaji uweze kufanyika kwa tija? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Aloyce John Kamamba Mbunge wa Jimbo la Buyungu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa lini uchimbaji mkubwa utafanyika katika maeneo yenye madini Wilayani kwake, napenda kumjulisha kwamba Taasisi yetu ya Utafiti wa Kijiolojia na Madini (GST) wanaendelea na utafiti katika maeneo mbalimbali nchini na pale wanapobaini kiwango cha madini yanayopatikana katika eneo husika wanaendelea kutangaza fursa za uwekezaji kwa wawekezaji wakubwa wenye mitaji mikubwa, ambao kimsingi wakija wanaingia katika ubia na wachimbaji wadogo walioko katika maeneo yale.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali lake la pili Wizara ya Madini tumeshaingia makubaliano na taasisi za kifedha za ndani ikiwepo Benki ya KCB, NMB, NBC, CRDB ya kuwapa wachimbaji wadogo mitaji waliokidhi vigezo ili waweze kuchimba madini hayo kwa tija. (Makofi)

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, Serikali ina taarifa juu ya madini yanayopatikana Kakonko na wananchi wananufaikaje nayo?

Supplementary Question 2

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kumuuliza Waziri Wilaya ya Mbogwe ina migodi midogo midogo inayomilikiwa na wachimbaji wadogo.

Je, Wizara imejipangaje kuwanufaisha wachimbaji hao wadogo ili kusudi na wao waone matunda kwenye Serikali yao?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika nchi yetu tuna wachimbaji wadogo katika sehemu mbalimbali, wenye leseni na moja ya kazi kubwa ya Wizara kupitia Taasisi zake za STAMICO na GST ni kuwajengea uwezo kwa kuwapa elimu juu ya Sheria ya Madini, Kanuni za Madini na namna ya uchimbaji bora pamoja na kuwatafutia fursa kwa wawekezaji wakubwa wanaokuja kutafuta madini katika maeneo ambayo yameshafanyiwa utafiti.

Mheshimiwa Naibu Spika, hatuishii hapo wachimbaji wadogo hawa pia tunaendelea kuwapelekea elimu ya kujiunga na kujisajili, waweze kufanya uchimbaji wenye tija kupitia taarifa za kijiolojia zinazoonesha madini yanayopatikana katika maeneo yao huko.