Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Madini 57 2022-09-16

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: -

Je, Serikali ina taarifa juu ya madini yanayopatikana Kakonko na wananchi wananufaikaje nayo?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Jimbo la Buyungu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa na Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (Geological Survey of Tanzania - GST), Wilaya ya Kakonko ina madini yafuatayo; dhahabu katika Kata za Nyamtukuza, Gwanumpu, Muhange na Kasuga. Pia ina madini ya vito aina ya Agate katika Kata za Gwanumpu na Kasanda na ina madini ya ujenzi katika Kata zote za Wilaya ya Kakonko.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Wizara imetoa leseni 27 za wachimbaji wadogo wa madini katika maeneo tofauti ya Kakonko kama ifuatavyo:- Dhahabu leseni 21, mawe ya chokaa leseni Mbili, shaba leseni Moja, kokoto leseni Tatu, mchanga leseni Moja, chuma leseni Moja na mawe leseni Moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na uwepo wa leseni za uchimbaji mdogo wa madini ambapo migodi huhitaji watu wengi wa kuzalisha, hivyo kwa njia hiyo wananchi wananufaika na ajira za moja kwa moja katika migodi kwa kutoa huduma mbalimbali kama chakula, malazi, usafirishaji na kadhalika, hivyo kuongeza manufaa ya kiuchumi kwa wananchi wa Wilaya husika na hususani kwa Wilaya ya Kakonko. Ahsante sana.(Makofi)