Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa banda la ukaguzi na kupokea samaki wabichi katika Kata ya Chifunfu utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa Mkandarasi huyu alipewa kazi hii toka mwaka jana Mei, 2021 na kazi yenye ilikuwa ni sehemu ya kutengeneza mwalo wa kupokelea samaki pamoja na vipimo vya samaki, hauoni sasa muda tayari umeshafika zaidi ya mwaka mmoja na miezi minne, ni lini sasa kazi hiyo ya ujenzi wa banda hilo utakamilika? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili la nyongeza ni kwamba, Mheshimiwa Naibu Waziri alifika katika eneo hilo la mradi na pamoja na kutembelea eneo hilo alikwenda pia kuangalia mabwawa ya kunyweshea mifugo katika Jimbo la Sengerema, lakini mpaka leo hii mabwawa hayo hayajapata fedha. Je, ni lini fedha zitaletwa kwa ajili ya kuyaziba mabwawa tisa yaliyopasuka katika Jimbo la Sengerema?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Tabasamu, Mbunge wa Sengerema, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu wa kukamilisha unafanyika kwa haraka mara baada ya kuvunja mkataba, hivi sasa wataalam wetu wapo kazini kuhakikisha kwamba kazi ile ya wananchi inakamilika ili waweze kupata huduma wanayostahiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili anataka kujua juu ya mabwawa yake lini yatapata fedha. Tayari kwa utaratibu wa Sheria ya Manunuzi tumekwishatangaza tenda na tupo katika hatua ya kupata wakandarasi na hatimaye yale yaliyopangiwa kwenye jimbo lake yatapata fedha na wakandarasi watatekeleza kazi yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimshukuru Mheshimiwa Tabasabu kwa ushirikiano mkubwa anaotupatia, ahsante sana.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa banda la ukaguzi na kupokea samaki wabichi katika Kata ya Chifunfu utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Hapa siku za karibuni tumesikia taarifa kupitia vyombo vya habari kwamba uhifadhi wa samaki hapa nchini kwenye baadhi ya maeneo, samaki wanahifadhiwa kwa kutumia dawa za kuhifadhia maiti, jambo ambalo linaleta taharuki kwa wananchi na wananchi hawajui nini cha kufanya ili wasipate hao samaki waliohifadhiwa kwa namna hiyo.

Je, ni nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha samaki hao hawahifadhiwi kwa vitu hivyo ambavyo vinasababisha kansa kwa Watanzania? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili alilolisema Mheshimiwa Paresso ni hypothesis halina hakika hadi sasa hivi. Ni kwamba watu wanahisia kuwa kiko kitu cha namna hiyo na ndiyo maana Mheshimiwa Makamu wa Rais alipokuwa Jijini Mwanza aliagiza Wizara ya Afya ifanye utafiti ili kama ni kweli kinafanyika kitu cha namna hiyo basi kizuiwe mara moja. Naomba niwatoe hofu Watanzania hakuna jambo linalohusu tuchukue samaki kutoka Mwanza tulete Dodoma au tupeleke Dar es Salaam kwa kuhifadhi na maji ya maiti, halipo jambo la namna hiyo! Naomba wawe na uhakika ya kwamba samaki wanaovuliwa na wavuvi wetu na wanaokwenda katika masoko mbalimbali wako salama hawana shaka yoyote. Ahsante sana. (Makofi)