Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 4 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 54 2022-09-16

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa banda la ukaguzi na kupokea samaki wabichi katika Kata ya Chifunfu utakamilika?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tabasam Hamis Mwagao, Mbunge wa Sengerema, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa banda la kupokelea samaki Chifunfu uliopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ulianza mwezi Mei, 2021 chini ya Mkandarasi M/S Fast Construction Company Limited ya Mkoani Mwanza kwa thamani ya shilingi 124,592,064.00 ambapo hadi sasa ujenzi umefikia hatua ya kuezeka na Mkandarasi ameshalipwa kiasi cha shilingi 95,768,193.00.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya ujenzi wa banda hilo ilipangwa kukamilika ndani ya kipindi cha miezi sita, hata hivyo Mkandarasi hakuweza kukamilisha kazi hiyo kwa mujibu wa mkataba, hivyo Serikali imechukua hatua za kusitisha Mkataba wa Mkandarasi huyo na hatua zingine za kisheria zinaendelea dhidi yake.