Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Uwanja wa Michezo katika Mji wa Lushoto?

Supplementary Question 1

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Lushoto kuna uwanja wa muda mrefu sana lakini uwanja ule unatakiwa ukarabati. Je, nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba inapeleka fedha kwa ajili ya ukarabati uwanja ule?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa michezo ni ajira. Je, Serikali ina mpango mkakati gani wa kuibua, kubaini na kuwahakiki vijana ambao wanataaluma ya michezo hususan Wilaya ya Lushoto hasa Lushoto Vijijini? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kunipa nafasi na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shekilindi, Mbunge wa Lushoto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Shekilindi swali lake la kwanza amependa kufahamu ni lini Serikali inatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa uwanja huo wa Lushoto lakini viwanja vingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika majibu yangu ya msingi nimeeleza kwamba Sera yetu ya michezo imezitaka Serikali kwa ngazi zote Serikali Kuu lakini Serikali za Mitaa kutenga fedha. Ni rahisi sana kama halmashauri zetu, Wakurugenzi pamoja na Waheshimiwa Wabunge na Madiwani tukasimamia kupitia Idara ya Michezo fedha zikatengwa na viwanja hivi vitajengwa na ninyi ni mashahidi tumeanza sisi kwenye wizara bajeti iliyopita tumetenga zaidi ya bilioni 10 kwa ajili ya kujenga viwanja vya kitaifa. Kwa hiyo, naomba nitoe rai tuendelee kutenga fedha kwa Serikali kwa ngazi zote ili tujenge viwanja hivi.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili Mheshimiwa Shekilindi amependa kufahamu ni jinsi gani tunashirikiana na TAMISEMI pia kuhakikisha vipaji vinaibuliwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi Wizara tumeshatoa maelekezo kwa ngazi zote na kwa vyama vyetu na mashirikisho, kwamba vipaji vinapoibuliwa vyama na mashirikisho yaweze kushiriki. Naomba nipongeze kwa niaba ya Waziri, Wabunge na Madiwani ambao wamekuwa wakichezesha ligi mbalimbali katika maeneo yao, maana yake wanaibua vipaji. Sisi kama Wizara tunakuja na mtaa kwa mtaa kuhakikisha kwamba tunapofika kwenye lengo la Taifa la Taifa cup tunahakikisha kwamba huko chini vipaji vimeibuliwa. (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru; kwanza nimpongeza Mheshimiwa Naibu Waziri, Mheshimiwa Pauline Gekul kwa kujibu maswali vizuri. Ofisi ya Rais, TAMISEMI tunashirikiana vema na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo katika kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo imetuelekeza kupitia Sanaa, Michezo na Utamaduni tunatengeneza ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilitoa maelekezo kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Shule za Msingi na Sekondari kote nchini kuhakikisha maeneo yanapimwa na tunapata haTi kufika Disemba, 30; na nimeelekeza kopi ya hati ije Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili niweze kujiridhisha kila shule ya msingi na sekondari imepimwa na kupata hati. Tunafanya hivi ili kuhakikisha maeneo ya shule tunapunguza uvamizi ikiwemo maeneo ya michezo kwa maana ya viwanja vya michezo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nitumie nafasi hii kuwaagiza Wakurugenzi kufanya kipaumbele kwenye bajeti za Mamlaka za Serikali za Mitaa, kutenga fedha kwa ajili ya kujenga viwanja vya michezo ni moja ya vipaumbele katika kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Uwanja wa Michezo katika Mji wa Lushoto?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii niweze kuuliza swali la nyongeza. Serikali ina mpango gani kujenga uwanja wa michezo Mkoa wa Simiyu unaoendana na hadhi ya Mkoa? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa nafasi. Naomba nijibu swali la Mheshimiwa Midimu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye mikoa yetu tuna ma-RAS ambao ni wenyeviti wa michezo, lakini kwenye wilaya zetu tuna ma-DAS ambao ni wenyeviti wa michezo, lakini tuna Wakurugenzi wetu tuna Maafisa Michezo kama ambavyo nimejibu kwenye majibu yangu ya msingi kwamba ni jukumu sasa Serikali za Mitaa wakatenga bajeti.

Mheshimiwa Naibu Spika, hili jambo linapaswa lianze haraka ili wananchi ambao wana vipaji vyao viendelee kuibuliwa kwa kucheza katika viwanja ambavyo ni vizuri. Kwa hiyo, nitoe rai kwa Mkoa wa Simiyu kutenga fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi huo. (Makofi)

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Uwanja wa Michezo katika Mji wa Lushoto?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Serikali haijawekeza sana kwenye viwanja vya masumbwi na kupelekea wanandondi kufanya mazoezi kwa kutumia njia za asili ikiwemo matairi. Je, ni lini Serikali itawekeza kujenga maeneo sahihi ambayo wanamasumbwi hao waweze kufanikiwa kama kijana wetu Mwakinyo anavyofanya? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa nafasi naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Mwakagenda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mwakagenda pamoja na Wabunge wengine wote kuhakikisha kwamba mchezo huu wa ngumi unafika mbali. Nimhakikishie kwamba, miongoni mwa maelekezo ambayo tunatoa katika nyanja mbalimbali na katika mashirikisho ni kuhakikisha kwamba miundombinu inajengwa, kwa sababu kila chama cha mchezo kina jukumu kwa mujibu wa sera yetu kuhakikisha vijanja na miundombinu inajengwa. Kwa hiyo, sisi tutaendelea kusimamia kama wizara kuhakikisha kwamba hayo maeneo yanapatikana. (Makofi)