Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 4 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 53 2022-09-16

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Uwanja wa Michezo katika Mji wa Lushoto?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Lushoto kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sera ya Maendeleo ya Michezo ya Taifa ya mwaka 1995 ibara ya 7(i) – (vii), jukumu la ujenzi na uendelezaji wa miundombinu ya michezo ni jukumu la Serikali Kuu, Mamlaka ya Serikali za Mitaa pamoja na Wadau wa Sekta ya Michezo zikiwemo Taasisi, Mashirika na Watu Binafsi. Hivyo, napenda kuzikumbusha na kuzielekeza halmashauri zote nchini ikiwemo Halmashauri ya Mji wa Lushoto kuzingatia matakwa ya Sera ya Michezo kwa kutenga fedha kutoka katika mapato ya ndani kwa ajili ya kujenga na kukarabati miundombinu ya michezo kwenye maeneo yao. Ahsante.