Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, ni lini Maboma ya Zahanati Vijiji vya Lata, Ikigijo, Lukale, Malwilo, Bulyanaga, Shushuni, Nata, Usiulize na Igushilu yatakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali. Msingi wa uanzishwaji wa maboma ya zahanati ulitokana na uliokuwa mradi wa uendelezaji wa mitaji katika Serikali za Mitaa. Hivyo katika Bunge la Kumi na Moja, lilitaka Serikali kukamilisha maboma hayo baada ya mradi huo kwisha. Je, Serikali haioni haja ya kupeleka mwongozo wa matumizi ya fedha katika fedha za kukamilisha maboma ya zahanati? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, takribani ni miaka miwili sasa Serikali imepeleka fedha 2021/2022: Je, Serikali iko tayari kufanya sensa ya kuangalia fedha zilizopelekwa kukamilisha maboma, zinaendana na maboma yaliyokamilishwa? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Leah Jeremiah Komanya, Mbunge wa Jimbo la Meatu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilipeleka mwongozo wa namna ambavyo fedha zinazopelekwa kwa ajili ya kukamilisha maboma ya zahanati Shilingi milioni 50 kwa kila boma zinatakiwa kutumika na kukamilisha maboma yale. Moja ya maelekezo ilikuwa ni kwamba, boma ambalo linaombewa fedha, Shilingi milioni 50 lazima liwe limefika hatua ya renter, siyo msingi au chini ya renter. Hesabu zilifanywa kwamba Shilingi milioni 50 ipelekwe kwenye jengo ambalo limefikia hatua ya renter linakamilika na kuanza kutoa huduma za afya mara moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali kila inapopeleka fedha, inapeleka na mwongozo, na pia tunafuatilia kuona utekelezaji wa miradi hiyo kwa mujibu wa mwongozo uliopelekwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, kuhusiana na kufanya tathmini kama fedha ambazo zilipelekwa kwa ujenzi wa maboma zimekamilisha; katika mwaka wa fedha uliopita zaidi ya maboma 555 yamelekewa Shilingi milioni 50, lakini zaidi ya asilimia 85 mpaka Juni mwaka huu yalikuwa yamekamilika, na yako hatua za mwisho za kusajiliwa. Tunaendelea kufanya tathmini kuhakikisha fedha hizo zinaleta tija kwa wananchi.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, ni lini Maboma ya Zahanati Vijiji vya Lata, Ikigijo, Lukale, Malwilo, Bulyanaga, Shushuni, Nata, Usiulize na Igushilu yatakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Mbugani katika Jimbo la Tabora Mjini ina uhitaji mkubwa sana wa zahanati. Sijui Serikali ina mpango gani wa kuisaidia Kata hiyo ya Mbugani?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Emmanuel Mwakasaka, Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata hii ya Mbugani ambayo ina uhitaji wa zahanati, nitoe maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, kufanya tathmini kujiridhisha na vigezo vya kujenga zahanati ya kimkakati na baada ya hapo kuona mapato ya ndani, na pia kuleta maombi Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili kwa kutumia mapato ya ndani na Serikali kuu tuone uwezekano wa kutekeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.