Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 50 2022-09-16

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: -

Je, ni lini Maboma ya Zahanati Vijiji vya Lata, Ikigijo, Lukale, Malwilo, Bulyanaga, Shushuni, Nata, Usiulize na Igushilu yatakamilika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Leah Jeremiah Komanya, Mbunge wa Jimbo la Meatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 ilipeleka Shilingi milioni 200 katika Wilaya ya Meatu kwa ajili ya ukamilishaji wa Zahanati nne. Aidha, katika mwaka 2022/2023 Serikali imetenga Shilingi milioni 200 kutoka Serikali Kuu na Shilingi milioni 100 kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri kwa ajili ya ukamilishaji wa Zahanati za Mwandukisesa, Masanga, Mwanyahina, Mwabagashi na Ikigijo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024 kiasi cha Shilingi milioni 100 kitatengwa kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri kwa ajili ya ukamilishaji wa zahanati za Igushilu na Nata. Ahsante.