Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaridhia Mkataba Na.189 wa Kazi za Staha kwa Wafanyakazi wa Majumbani?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, kwanini Serikali isiridhie sehemu ya mkataba huo ambayo haina matatizo wala ukakasi ili kuwasaidia wafanyakazi wa majumbani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili: Serikali inawasaidaje wafanyakazi wa private sectors wakiwemo wa mahoteli na kwenye baa waweze kujiunga na vyama vya wafanyakazi ili kulinda maslahi yao?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Thea Medard Ntara, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba mambo ambayo hayana madhara yanayoendana na mila, tamaduni na desturi ya nchi yetu, tayari sheria yetu ya ajira na mahusiano kazini ya sura namba 366 imeshayazingatia hayo na tumeyafanyia domestication kwa maana ya kuchukua na kuyaweka kwenye sheria zetu za ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia katika eneo hilo, siyo mikataba yote ya Kimataifa ambayo tunairidhia kwa ujumla wake. Tuna haki kwa mujibu wa Sheria za Kimataifa ya kusaini tu, lakini kuna process nyingine ya kufanya ratification na baada ya hapo unaweza ukawa unafanya reservation. Kwa hiyo, tuna reservation kwenye baadhi ya vifungu vya Mkataba huu wa Kimataifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hilo, nimhakikishie Mheshimiwa tayari Serikali ina utaratibu mzuri wa kuhusiana na Mikataba ya Kimataifa kwenye masuala ya haki za wafanyakazi kwa mujibu wa Shirika la Kazi Duniani (International Labour Organization). Sambamba na hilo, tunaendelea kuratibu hata wale wafanyakazi wa majumbani walio nje nchi, kwa mfano, kwa nchi za Mashariki ya Kati, kule Oman, wako zaidi ya wafanyakazi 14,000 ambao walikuwa wanafanya kazi kule na 55 wako kwenye kada nyingine tofauti na ufanyakazi wa majumbani.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri, umejibu vizuri hilo swali, tuendelee.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili la kuhusiana na wafanyakazi wa hotelini kuingia kwenye vyama vya wafanyakazi, tunayo pia sheria inayohusiana na masuala ya Trade Unions ambayo ni sheria inayoratibu uwepo wa Trade Unions. Vyama hivi vya wafanyakazi wana haki ya kukusanya wanachama katika maeneo mbalimbali yaliyosajiliwa. Kwa hiyo, tayari utaratibu huo unafanyika na tumeshaanza kutembelea baadhi ya hoteli na maeneo mengine kuhakikisha wafanyakazi hawa wanapewa mikataba na kulinda haki zao za msingi. Ahsante.