Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 4 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 48 2022-09-16

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaridhia Mkataba Na.189 wa Kazi za Staha kwa Wafanyakazi wa Majumbani?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. PASCAL P.
KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Thea Medard Ntara, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Mkataba huu wa Kimataifa wa kuhusiana na haki za wafanyakazi wa majumbani haujaridhiwa ambapo Serikali inafanya tathmini ya kina kuona kama kuna umhimu wa kuridhia na kuwa masuala mengi yaliyoko katika Mkataba huu yanatekelezwa kwa mujibu wa Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini, Sura 366 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2019. Aidha, siyo kila Mkataba wa Kimataifa unaridhiwa. Tunaridhia mikataba ya msingi (Core Conventions) ambapo kwa Mikataba isiyo ya lazima (Other Conventions) uridhiaji wake utazingatia mila, desturi na hali ya uchumi wa nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kushauriana na wadau katika suala hili. Nitumie fursa hii kuwaomba wadau kuendelea kutoa maoni ya njia bora ya kuendelea kuboresha maslahi na haki za wafanyakazi wa majumbani kwa kuzingatia mila, desturi na hali ya nchi yetu. Ahsante.