Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - Je, ni yapi yalikuwa malengo ya Serikali kuanzisha Chuo cha Diplomasia?

Supplementary Question 1

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu hayo naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

(a) Je, wanafunzi wanaosoma Chuo cha Diplomasia wanafanya wapi mafunzo kwa vitendo ili sasa lengo la kuanzisha Chuo cha Diplomasia liwe limetimia?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Serikali imekubali kwamba yaliyokuwa malengo ya msingi kuanzia Chuo cha Diplomasia kwa sasa yamebadilika kutokana na mahitaji ya nchi na pia kutokana na masuala mengine ambayo Serikali wanajua kwanini walipadilisha.

(b) Je, ni kwanini sasa Serikali isione haja ya kupitia upya mfumo wa utoaji elimu kwenye chuo hiki ambacho lengo lake lilikuwa ni kutoa viongozi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwasababu hata wanaotolewa katika chuo hiki wahitimu wengi hawatumiwi kama ambavyo lengo la kuanzisha chuo hicho lilivyokuwa. Sasa ni kwanini wasipitie upya ili wanaohitimu katika chuo hicho wawe na tija kwa taifa na Serikali ifikie malengo yake inayosema kwamba inazalisha viongozi? Ahsante. (Makofi)

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nusrat Shaaban Hanje, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza ni kuhusu mafunzo kwa vitendo. Chuo hiki kimsingi kinapowatoa wale wanafunzi wanakwenda kwenye maeneo mbalimbali kwa ajili ya field zao, moja ya eneo ambalo wanapewa nafasi ni Wizara ya Mambo ya Nje yenyewe ambako wanafunzi wachache huwa wanapewa nafasi kutokana na ukweli wa uwezo wa Wizara yenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini maeneo mengine ni kwenye taasisi mbalimbali zenye sura ya Kimataifa, vile vile kule kwenye NGO na maeneo ambayo utendaji wake upo katika sura ya kimataifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la tija, ni kwamba chuo hiki kina tija kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi kwamba kwa sasa kimezalisha wanadiplomasia wengi sana ambao wanatumika katika maeneo mbalimbali. Na ukizingatia kwamba tuna hiki chuo kiliboreshwa na kufanyiwa maboresho ya uhakika kimekuwa na sura ya chuo kikuu, na sasa hivi kinatoa hadi shahada ya juu, kama nilivyoieleza hapo, wanatoa hadi masters pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ninachoweza kusema ni kwamba mafunzo wka vitendo wanapatiwa lakini vile vile tija inaonekana kwenye Nyanja za kimataifa na wasomi wengi sana tumekuwa tukiwatumia katika maeneo mbalimbali, ahsante.