Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 5 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 78 2022-09-19

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: -

Je, ni yapi yalikuwa malengo ya Serikali kuanzisha Chuo cha Diplomasia?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI
alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nusrat Shaaban Hanje Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Chuo cha Diplomasia hapo awali kilikuwa ni chuo cha kimkakati ambacho kilianzishwa kwa ushirikiano kati Tanzania na Msumbiji kwa lengo la kuwajengea uwezo viongozi mbalimbali katika nyanja za kidiplomasia na uongozi katika ngazi za kitaifa na kimataifa kutoka katika hizo nchi mbili. Kutokana na ubora cha chuo hiki Serikali ilifanya maboresho kwa kuongeza mitaala na kilianzisha kozi katika ngazi ya cheti, stashahada, shahada, stashahada ya uzamili na shahada ya uzamili ambazo zilianza kujumuisha wanafunzi kutoka nje ya mfumo wa watumishi wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi sasa chuo kimezalisha wanadiplomasia wengi ambao wameweza kuajiliwa katika Serikali yetu, sekta binafsi pamoja na jumuiya za kikanda na kimataifa. Hivyo, chuo kimefikia lengo lake baada ya kufanyika kwa maboresho husika na kuweza kuchangia kwa kiasi kikubwa katika maendeleo ya taifa letu na wananchi kwa ujumla.