Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, kuna manufaa gani ya kuunganisha Idara ya Kilimo na Mifugo katika Halmashauri za Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa katika ngazi ya Wizara, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ni Wizara mbili tofauti zenye majukumu tofauti. Katika mwaka wa fedha 2022/2023 ndiyo Wizara zilizopewa fedha nyingi za miradi, watendaji wa Wizara hizi wako katika halmashauri. Je, sasa kwa mfano Wizara moja inapotoa maelekezo halmashauri na kwenda kusimamiwa na mkuu wa idara nyingine, mfano Wizara ya Kilimo, kutoa maelekezo kwa Mkuu wa Idara ya Mifugo, je, hakutarudisha ufanisi wa utendaji wa kazi hiyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Idara hizi za Kilimo na Mifugo katika halmashauri ndizo zinazotegemewa kwa mapato ya ndani, sasa kumwachia majukumu mkuu wa idara moja kusimamia ukusanyaji wa mapato ya kilimo, mifugo na uvuvi, je, hakutaathiri ukusanyaji wa mapato katika halmashauri hizo? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Yustina Arcadius Rahhi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Wizara ya Kilimo na Wizara ya Mifugo ni Wizara mbili tofauti kwa ngazi ya Wizara, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara zikiwa tofauti haimaanishi kwamba coordination ya kuwatumia na kuwaelekeza Wakuu Idara katika Halmashauri inakwama. Halmashauri zetu zinatofautiana, kuna halmashauri ambazo zinashughuli nyingi zaidi za mifugo, kuna halmashauri nyingi zaidi ambazo ni za kilimo. Wakuu wa Idara wa Halmashauri hizo itazingatiwa halmashauri ina idadi kubwa zaidi ya shughuli gani, kama ni za kilimo, Mkuu wa Idara atakuwa ni Afisa wa Kilimo. Kama ni mifugo Mkuu wa Idara atakuwa ni mtaalam wa masuala ya mifugo na coordination ya Serikali ni moja mpaka chini bila kujali utofauti wa Wizara katika ngazi ya kitaifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na mapato ambayo yanakusanywa kutoka Idara ya Kilimo na Idara ya Mifugo, ikumbukwe kwamba wataalam wote wa mifugo wanaendelea kuwepo na Wakuu wa Idara kwa maana ya wataalam wetu wa kilimo wanaendelea kuwepo, kinachotofautisha ni mkuu wa idara lakini ataendelea kuwaratibu na kuwasimamia wataalam katika ukusanyaji mapato katika kusimamia shughuli za kilimo na mifugo kwa muktadha huo. Ahsante sana.