Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 70 2022-09-19

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE YUSTINA A. RAHHI aliuliza: -

Je, kuna manufaa gani ya kuunganisha Idara ya Kilimo na Mifugo katika Halmashauri za Wilaya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekit, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yustina Arcadius Rahhi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchakato wa uandaaji wa muundo na mgawanyo wa majukumu huzingatia mambo mbalimbali ikiwemo Sera, Sheria na maelekezo ya Serikali ya wakati husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Muundo na Mgawanyo wa Majukumu ya Halmashauri za Wilaya uliidhinishwa rasmi tarehe 29 Januari, 2022, baada ya kufanya mapitio kwa kushirikisha wadau mbalimbali. Katika mabadiliko hayo, Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika na Idara ya Mifugo na Uvuvi iliunganishwa na kuwa Idara moja ya Kilimo na Mifugo kutokana na kushabihiana kwa majukumu ya Idara ya Kilimo na Mifugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, manufaa ya kuhuisha miundo katika ngazi ya halmashauri na Mikoa ni kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa majukumu, kupunguza gharama za uendeshaji na kuimarisha uratibu na usimamizi. Hivyo, muundo mpya wa halmashauri umepungua kutoka Idara 13 na Vitengo Sita na kuwa na Idara Tisa na Vitengo Tisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Muundo na Mgawanyo wa Majukumu wa Taasisi hizo unaweza kufanyiwa mabadiliko inapohitajika bila kuathiri ufanisi ili kukidhi utendaji kazi wa kila siku. Ahsante.