Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE K.n.y. MHE. ABUBAKARI D. ASENGA) aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapima upatikanaji wa madini ya dhahabu katika Jimbo la Kilombero na maeneo jirani ya Mlima Udzungwa?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Abubakar Assenga, Mbunge wa Kilombero, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kutokana na utafiti uliofanywa na GST na kubaini kwamba, katika maeneo husika madini yapo. Je, Serikali iko tayari sasa kuendelea na utafiti katika maeneo mengine jirani ambapo madini hayakupatikana?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kwenda Jimboni Kilombero katika maeneo ambayo madini hayo yanapatikana au kumekuwa na dalili za uwepo wa madini ili kwenda kujenga uelewa zaidi kwa wananchi wanaozunguka maeneo hayo? Ahsante.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ally Kassinge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kwenda kufanya utafiti katika maeneo mengine, jibu ni ndio. Wizara inaendelea kupitia taasisi yake ya GST kufanya utafiti katika maeneo yote ya nchi yetu kubaini maeneo yenye madini ya aina mbalimbali, ili tuweze kuyafahamu na kuweza kuwagawia wachimbaji wadogo na wawekezaji kutoka sehemu mbalimbali katika dunia kwa sababu, Rais wetu naye alitusaidia sana kupitia Royal Tour kuyatangaza na wawekezaji wanazidi kumiminika nchini kwa hiyo, zoezi la utafiti linaendelea nchi nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili la mimi kwenda Kilombero na kuendelea kuangalia maeneo yaliyopatikana kwa ajili ya wachimbaji wadogo, ndio, niko niko tayari kutembelea katika maeneo hayo. Nipende tu kumjulisha kwamba, hata sasa katika maeneo ambayo madini yameshabainika tuna zaidi ya leseni 22 za wachimbaji wadogo ambao wanaendelea na tafiti na uchimbaji wa madini ya vito pamoja na madini ya dhahabu.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE K.n.y. MHE. ABUBAKARI D. ASENGA) aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapima upatikanaji wa madini ya dhahabu katika Jimbo la Kilombero na maeneo jirani ya Mlima Udzungwa?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiacha eneo la Liganga na Mchuchuma, eneo la Njombe kwa ujumla mpaka maeneo ya Mufindi hayajafanyiwa utafiti kabisa. Pamoja na kueleza kwamba, nchi nzima inafanyiwa utafiti ni lini sasa Serikali itaifanya GST ianze utafiti kwenye maeneo ya Njombe ambayo hayajafanyiwa utafiti?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwanyika, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika Nyanda za Juu Kusini hasa Mikoa ya Ruvuma, Njombe na hususan kule Ludewa, kuna maeneo makubwa sana yenye madini ya chuma na madini ya makaa ya mawe. Wizara inaendelea kuchakata kwa kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Uwekezaji utaratibu mzuri wa kuwapata wawekezaji wakubwa wa kuyachimba madini hayo, lakini pia, tuko katika hatua za mwisho kabisa za kubainisha maeneo ya kuwagawia wachimbaji wadogo ili madini hayo yaweze kuleta tija kwa Taifa letu na raia wake.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE K.n.y. MHE. ABUBAKARI D. ASENGA) aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapima upatikanaji wa madini ya dhahabu katika Jimbo la Kilombero na maeneo jirani ya Mlima Udzungwa?

Supplementary Question 3

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Huu ukanda wa Milima ya Udzungwa unaelekea kwa kiwango kikubwa kwenye Wilaya ya Kilolo na huu ukanda unaungana na Kata ya Udekwa na Kata ya Ukwega ambayo pia, inaaminika kuwa na madini. Je, Wizara iko tayari kutuma wataalam kufanya utafiti ili kama madini hayo ya dhahabu yapo, kama ilivyo kule Ulanga, yaweze pia kuchimbwa?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nyamoga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama nilivyotangulia kusema, kama Wizara ya Madini, kupitia taasisi zake GST na hata STAMICO, tuko katika mpango mahususi wa kuendelea kufanya utafiti wa kubaini maeneo yote yenye madini nchini na itahusisha pia, eneo lake na sehemu alizozitaja kwa sababu, lengo letu kama Taifa ni kuhakikisha kwamba, rasilimali madini inakwenda kuzalishwa ili iletee Taifa letu tija. Nimhakikishie kwamba na nitumie pia nafasi hii kuiagiza taasisi yetu ya GST katika mpango kazi wao wa mwaka huu waweke katika utaratibu na ratiba safari ya kuelekea kule kufanya utafiti kwenye eneo la Mheshimiwa Mbunge.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE K.n.y. MHE. ABUBAKARI D. ASENGA) aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapima upatikanaji wa madini ya dhahabu katika Jimbo la Kilombero na maeneo jirani ya Mlima Udzungwa?

Supplementary Question 4

MHE. ENG. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Wilaya ya Hanang, Kata ya Basutu, tuna mgodi wa dhahabu, lakini uzalishaji wake uko chini sana. Je, Serikali iko tayari kushirikiana na mwekezaji ili kuongeza uzalishaji wa dhahabu kwenye eneo hilo? (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Wizara, tunashirikiana na wawekezaji na wachimbaji wadogo. Vilevile sisi kama Wizara lengo letu kubwa ni kusimamia upande wa sera, kanuni na sheria, lakini pia kutoa elimu na kuwasaidia wachimbaji wadogo kupata fursa za kufikia taasisi za kifedha ili waweze kukopeshwa vifaa ama fedha baada ya kukidhi vigezo ili uzalishaji uweze kuendelea na waweze kupata tija kwa juhudi ya uchimbaji wa madini.