Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Madini 91 2022-09-20

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE K.n.y. MHE. ABUBAKARI D. ASENGA) aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapima upatikanaji wa madini ya dhahabu katika Jimbo la Kilombero na maeneo jirani ya Mlima Udzungwa?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Damian Assenga, Mbunge wa Jimbo la Kilombero, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kupitia Taasisi yake ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), imefanya utafiti wa awali na kuchora ramani kwenye maeneo yote yaliyoko katika Jimbo la Kilombero katika mfumo wa Quarter Degree Sheet (QDS). Tafiti hizi za awali zinaonesha kuwa kuna uwepo wa madini ya dhahabu na madini ya vito katika Kata ya Chisano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, GST pia ilifanya utafiti wa awali na kuchora ramani ya eneo la Hifadhi ya Milima ya Udzungwa na maeneo jirani. Hata hivyo, utafiti umeonesha kwamba, hakuna taarifa zozote za uwepo wa madini ya thamani katika milima hiyo. Ahsante.