Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuweka mita janja za maji ili watumiaji wachague kutumia kulingana na matumizi?

Supplementary Question 1

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naipongeza Wizara kwa kazi kubwa wanayoifanya kwenye sekta ya maji na nina swali moja la nyongeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia ambayo yanachagiza huduma za kijamii kufika viganjani mwa watumiaji. Je, Wizara haioni umuhimu wa kuweka mpango kazi mahususi, yaani ikifika 2025 mita hizi janja ziweze kutumika na watu majumbani?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Judith Kapinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe taarifa kwamba, tayari Wizara imeshakuwa na huo mpango na tayari umeshaanza kutekelezwa. Baadhi ya sisi hapa ndani pia tutakuwa mashahidi, hata mimi mwenyewe nyumbani kwangu natumia prepaid meter, kwa hiyo, sio kwamba, bado watu hawajaanza kutumia majumbani, tayari tumeanza, lakini kwa kuangalia kama modules za kufanya tu utafiti kuona kwamba, ufanisi wake umekaaje, lakini mpaka kufika hiyo 2025 anayoongelea Mheshimiwa Mbunge, nimtoe hofu jamii kubwa sana itakuwa tayari inatumia prepaid meters.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuweka mita janja za maji ili watumiaji wachague kutumia kulingana na matumizi?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na ningependa kujua, Serikali ina bei maalum elekezi ya unit moja ya maji kwa sababu, kila halmashauri inajipangia bei na mwisho wa siku mzigo unabaki kwa mwananchi; kwa mfano Bunda, unit moja 1,800/= ukienda maeneo mengine ni 1,000/= mpaka chini ya 1,000/=. Je, hamwoni kuna haja ya kupanga bei maalum ili kuwaondolea mzigo wananchi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari Wizara ilishatangaza kupitia Waziri mwenye dhamana, bei elekezi kwenye maeneo yote ilishatangazwa. Bei hazifanani kulingana na uwekezaji wa miradi. Mradi ambao unatumia source ya kusuma maji kama ni diesel, bei yake haiwezi kufanana na inayosukuma maji kwa kutumia umeme wa TANESCO, tofauti na bei ambapo maji kutoka katika chanzo chake yatakuwa yanasukumwa na umeme wa jua, lakini vilevile ukubwa wa mradi kulingana na jiografia ya eneo ulipo huo mradi. Hivyo, bei haziwezi kufanana, lakini bei elekezi tayari zimetolewa kulingana na mradi namna ambavyo ulitengenezwa.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuweka mita janja za maji ili watumiaji wachague kutumia kulingana na matumizi?

Supplementary Question 3

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante:-

Mheshimiwa, Mwenyekiti, hivi karibuni Mheshimiwa Waziri wa Maji alifanya ziara Wilayani Monduli, Mkoa wa Arusha na kuahidi mradi mkubwa wa maji utakaoanzia katika tanki ya gari popo, utakaonufaisha vijiji 12 vya Kata ya Meserani, Lepurko, Moita na kata nyingine. Je, ni lini hasa mradi huu mkubwa wa maji utaanza rasmi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine Magige, Mbunge Viti Maalum, Arusha, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli mradi huu upo kwenye mpango wa Wizara, kama alivyoelekeza Mheshimiwa Waziri na wakati wowote ule mradi unaenda kuanza. Tunasubiri tu mafungu yakae vizuri, mradi unakuja kutekelezwa na tutahakikisha vijiji vyote 12 vinafikiwa na maeneo yote ya karibu ambayo bomba kuu litapita kwenye mradi huu yatakwenda kunufaika.