Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 90 2022-09-20

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuweka mita janja za maji ili watumiaji wachague kutumia kulingana na matumizi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Judith Salvio Kapinga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuboresha utoaji wa huduma ya maji na watumiaji kulipa gharama kulingana na matumizi, Serikali imeshaanza kutumia mita za malipo kabla ya matumizi (water prepaid meter) katika maeneo tofauti tofauti ikiwemo katika Mamlaka ya Maji Iringa, Arusha, Tanga, Singida, Mwanza, Mbeya, Kahama na Mtwara. Aidha, mita hizo pia zimefungwa kwenye maeneo ya taasisi kama vile shule, hospitali na Majeshini wakati Serikali ikiendelea kujiridhisha na ufanisi wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa kufunga mita za malipo kabla ya matumizi (water prepaid meter) utafanyika kwa awamu ili kuweza kufikia maeneo mbalimbali katika mikoa yote nchini. Aidha, jitihada hizi zinaenda pamoja na kuhakikisha mamlaka za maji zinatumia mfumo wa malipo kutoa ankra za maji kulingana na matumizi ya wateja (unified billing system).