Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupandisha hadhi barabara ya Tunduru – Namasakata – Misechela kuwa ya Mkoa?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, ni kweli barabara hii kwa muda mrefu imekuwa na shida na haipitiki, ni barabara ambayo ni ya ulinzi, inaunganisha kati ya Msumbiji na Tanzania. Kwa mazingira yaliyoko Msumbiji, barabara hii ni muhimu itengenezwe kwa sababu kipindi cha kifuko haiptiki kabisa: -

Je, ni lini sasa Waziri wa TAMISEMI, au Naibu wake wataenda katika eneo hili kuangalia hii kero ambayo inapatikana katika eneo lile? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili: Kwa kuwa barabara hii iliweza kupitishwa kwenye michakato mbalimbali kabla TARURA haijaanzishwa; na baada ya TARURA kuanzishwa, barabara hii ikabaki kwenye TARURA peke yake; na maombi yale yalifika mpaka kwenye RCC: Je, lini Serikali itaangalia ma-file yake kuona mapendekezo yale ili yaweze kupitishwa kwa haraka kunusuru hali iliyoko pale Msumbiji? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Daimu Idd Mpakate, Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tuko tayari Kwenda katika jimbo lake muda wowote na tuko flexible kwa sababu huo ndiyo wajibu wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni kwamba, jukumu la kupandisha hadhi hizi barabara liko chini ya TANROADS kupitia Wizara ya Ujenzi. Kwa hiyo, nafikiri kwa sababu Serikali tunafanya kazi kwa pamoja, tutaendelea kushirikiana kuhakikisha kwamba jambo hili linafanyika kwa haraka. Ahsante sana.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupandisha hadhi barabara ya Tunduru – Namasakata – Misechela kuwa ya Mkoa?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya kutoka Mlalo kwenye Ngwelo, Mlola, Mashewa hadi Korogwe inaunganisha wilaya mbili; na barabara hii iko chini ya wakala wa barabara vijijini kwa maana ya TARURA na imeshaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kwa kilomita 2.7: Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuipandisha hadhi hii barabara na kuwa ya mkoa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Rashid Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua kazi nzuri ambayo inafanyika katika Jimbo la Mlalo, hususan hii barabara ya Mlalo – Nachiwa mpaka Korogwe na ndio maana sisi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, tulitenga fedha kwa ajili ya kuanza sasa kutekeleza kwa ujenzi wa lami. Sasa kwa kuwa, maombi yao ni kupandisha hadhi, nafikiri tutaiagiza Halmashauri ya Mlalo ifuate taratibu kama ambavyo tumeiagiza Halmashauri ya Tunduru, ili barabara hiyo nayo iweze kufikia hivi viwango ambavyo Mheshimiwa Mbunge anahitaji. Ahsante sana.